Rais Samia amlilia Lawrence Mafuru

November 9, 2024 1:59 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni baada ya kufariki Novemba 9, 2024 akipatiwa matibabu nchini India.

Arusha.  Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha aliyekuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Lawrence Nyasebwa Mafuru aliyefariki leo Novemba 9, 2024.

Taarifa ya Ikulu Mawasiliano inabanisha kuwa  Mafuru amefariki leo Novemba 9, 2024 katika Hospitali ya Apollo nchini India alipokuwa akipatiwa matibabu.

Kupitia taarifa yake iliyochapishwa kwenye mitandao ya kijami Rais Samia ametoa pole kwa watumishi wa Tume ya Mipango, ndugu, jamaa na marafiki.

“Ninatoa pole kwa familia, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji) Mheshimiwa Prof. Kitila Alexander Mkumbo, watumishi wa Tume ya Mipango, ndugu jamaa na marafiki kufuatia msiba huu…

…Mafuru atakumbukwa kwa utumishi wake uliotukuka, bidii na ubunifu alipotumikia nafasi mbalimbali ndani ya Serikali,” amesema Rais Samia katika mitandao yake ya kijamiai ikiwemo Instagram.

Enzi za uhai wake Mafuru alitumikia nafasi mbalimbali katika Serikali za awamu tofauti ikiwemo ya Rais Samia kama Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango ya Taifa nafasi aliyoitumikia tangu Julai 5, 2023 tume hiyo ilipoundwa.

Kabla ya kuitumikia nafasi hiyo Mafuru alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango (Usimamizi wa Uchumi). 

Pia aliwahi Mkurugenzi wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Msajili wa Hazina na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi  katika Serikali ya awamu ya nne ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Nukta TV

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

Nukta TV

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Nukta TV