Ndege ya Tanzania iliyokamatwa Canada yaachiliwa, kutua Mwanza
- Rais Magufuli athibitisha kuwa imeachilia na itarejea nchini hivi karibuni.
- Ndege hiyo itakapowasili nchini itapokelewa katika uwanja wa ndege jijini Mwanza.
Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, John Magufuli amesema ndege ya Tanzania aina ya Bombardier Q400 iliyokuwa imekamatwa nchini Canada imeachiwa na wananchi watatangaziwa siku ya kuwasili ili waipokee jijini Mwanza.
Rais Magufuli aliyekuwa akizungumza na wajumbe wa Halmasharuri kuu ya Taifa ya chama cha Mapinduzi leo (Desemba 12, 2019) jijini Mwanza siku ya ndege hiyo kurudi na kupokelewa itatangazwa hapo baadaye.
Hata hivyo, amesema ndege hiyo itakapowasili nchini itapokelewa katika uwanja wa ndege jijini Mwanza.
“Kwa taarifa tu ndege yetu iliyokuwa imeshikwa Canada imeachiwa, mtatangaziwa tarehe ya kuipokea na mtaipokelea hapa Mwanza,” amesema Rais
Soma zaidi:
- Waziri azungumzia ndege za ATCL kuchelewa, kuahirisha safari
- Shirika la ndege la Ethiopia limesitisha safari zote za ndege aina ya Boeing 737
- ATCL inavyojitanua kimataifa
Mamlaka nchini Canada zilikamata ndege hiyo, kutokana na shauri la kesi iliyofunguliwa na mkulima mstaafu raia wa Namibia, Hermanus Steyn.
Steyn pia alifungua kesi nchini Afrika Kusini mwezi Agust iliyosababisha ndege aina ya Air Bus 220-300 izuiliwe na hatimaye serikali ya Tanzania kushinda kesi mahakamani
“Mhe. Rais ndege yetu aina ya Bombadier ambayo ilipaswa ifike Tanzania kutokea Canada imekamatwa na mtu yule yule ambaye aliikamata ndege yetu kule Afrika ya Kusini.” alisema Prof. Kabudi, Novemba 23 jijini Dodoma katika hafla ya kuapishwa kwa mabalozi.
Latest
