Ndege nyingine yaanguka, yaua wawili Tanzania

September 23, 2019 7:17 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Ndege ya Kampuni ya Auric Air imeanguka leo asubuhi katika uwanja mdogo wa ndege Seronera uliopo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. 

Ajali hiyo imetokea leo (Septemba 23, 2019) majira ya 1:30  asubuhi ambapo watu wawili wamepoteza maisha akiwemo rubani mmoja na abiria mmoja. 

Kwa mujibu wa taarifa ilitolewa na Mamlaka ya hifadhi za Taifa (Tanapa), rubani na abiria wote ni raia wa Tanzania na kueleza kuwa taarifa kuhusu ajali hiyo zitatolewa baadaye.

Hii ni ndege ya tatu kuanguka na kusababisha vifo na majeruhi ndani ya kipindi cha miezi mitatu ambapo nyingine ilitokea mkoani Tabora na kisiwa cha Mafia mkoani Pwani.

Agosti 6, 2019, ndege ndogo ya abiria (5H-NOW) ya kampuni ya Tropical iliyokuwa inatokea katika kisiwa cha Mafia kuja jijini Dar es Salaam ilianguka na kuwaka moto maeneo ya Mafia, ambapo watu tisa walinusurika kifo. 

Pia Agosti 3 mwaka huu, ndege ya usaidizi ya mradi wa wanafunzi wa Afrika Kusini ya U-Dream ilianguka dakika moja baada ya kupaa angani kutoka katika uwanja wa ndege uliopo kijiji cha Igigwa Wilayani Sikonge mkoani Tabora magharibi mwa Tanzania. 

Ndege hiyo ilikuwa inaendeshwa na raia wa Afrika Kusini, Des Werner na Wener Froneman kutoka Cape Town kuelekea Cairo Misri ambapo wote wawili walipoteza maisha.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV