Nchi 5 zinazoongoza kwa maambukizi ya Uviko-19 Afrika
Dar es Salaam. Licha ya hatua mbalimbali kuchukuliwa kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa Uviko-19 ikiwemo utoaji wa chanjo, ugonjwa huo bado upo na unaendelea kuua watu.Â
Nchi ya Afrika Kusini kwa mujibu wa takwimu za Septemba 28, 2022 zilizotolewa na Shirika la Afya Duniani (WHO) ndiyo inaongoza kwa maamukizi ya kiwango cha juu barani Afrika.
​WHO inaeleza kuwa hadi jana, watu milioni 4.02 walikuwa wameambukizwa Uviko-19 huku 102,169 wakifariki dunia.
