Mwelekeo mpya mapambano magonjwa ya milipuko duniani

November 22, 2022 12:31 pm · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Wanasayansi kujichimbia kufuatilia vimelea vya magonjwa hayo.
  • Magonjwa kama Uviko-19, Ebola na Marbug kupewa kipaumbele.  

Dar es salaam. Wakati mataifa mbalimbali duniani yakiendelea  kukabiliana na magonjwa ya milipuko ambayo yamesababisha athari nyingi kiuchumi na kijamii ikiwemo Uviko-19 na Ebola, wanasayansi wanafikiria kuja na suluhu ya kuepusha kabisa magonjwa hayo kwa siku za usoni.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti ya Shirika la Afya Duniani (WHO) jana Jumatatu Novemba 21, 2022, shirika hilo lipo mbioni kuzindua mchakato wa kufuatilia vimelea ambavyo vinaweza kusababisha magonjwa ya milipuko.

Ufuatiliaji huo utafanywa na jopo la wanasayansi zaidi ya 300 ambao watafuatilia familia za bakteria na virusi 25 na kisha watapendekeza ni vimelea vipi vipewe kipaumbele zaidi.


Soma zaidi:


Mchakato huo utahusisha vigezo vya kisayansi vinavyohusiana na athari za kijamii na kiuchumi ambapo unatarajiwa utachochea maendeleo ya tafiti katika upatikanaji wa tiba pamoja na chanjo.

“Ni muhimu kuwa na mchakato huu hususan linapotokea janga linalohitaji majibu ya haraka kama Uviko-19, isingekuwa rahisi kupambana nao kwa haraka kama kusingekuwa na hatua kama hizi,” anasema Dk Michael Ryan, Mkurugenzi wa Mpango wa Dharura wa WHO.

Magonjwa kama Ebola, Uviko-19, Marbug, homa ya Lassa, homa ya bonde la ufa pamoja na zika ni miongoni mwa maradhi yaliyopo katika orodha ya magonjwa yatakayopewa kipaumbele katika utafiti huo.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.