Mtumbwi waua shabiki wa Yanga, watano hawajulikani
Mwanza. Mtu mmoja amefariki dunia huku wengine watano wakiwa hawajulikani walipo baada ya mtumbwi waliokuwa wanasafiria kuingia maji na kuzama ndani ya Ziwa Victoria usiku wa kuamkia leo wakitoka kusherehekea wiki ya Mwananchi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Wilbroad Mutafungwa amesema hadi mtumbwi huo unazama uilikuwa na watu 23 ambao ni mashabiki wa timu ya mpira wa miguu ya Yanga ambao walikuwa wanatoka kusherehekea kilele cha Wiki ya Mwananchi wilayani Sengerema.
Mutafungwa amewaambia wanahabari jijini Mwanza kuwa watu wengine 17 waliokuwepo kwenye mtumbwi huo walinusurika na ajali hiyo.
“Watu hao walikuwa wanasafiri kutoka kisiwa cha Yozu kuelekea kisiwa cha Bulyaheke wilayani Sengerema ndipo mtumbwi huo ulipoanza kuingia maji na kusababisha kuzama,” amesema Mutafungwa.
Latest