Mtumbwi waua shabiki wa Yanga, watano hawajulikani

August 6, 2024 5:42 pm · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link

Mwanza. Mtu mmoja amefariki dunia huku wengine watano wakiwa hawajulikani walipo baada ya mtumbwi waliokuwa wanasafiria kuingia maji na kuzama ndani ya Ziwa Victoria usiku wa kuamkia leo wakitoka kusherehekea wiki ya Mwananchi. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Wilbroad Mutafungwa amesema hadi mtumbwi huo unazama uilikuwa na watu 23 ambao ni mashabiki wa timu ya mpira wa miguu ya Yanga ambao walikuwa wanatoka kusherehekea kilele cha Wiki ya Mwananchi wilayani Sengerema.

Mutafungwa amewaambia wanahabari jijini Mwanza kuwa watu wengine 17 waliokuwepo kwenye mtumbwi huo walinusurika na ajali hiyo. 

“Watu hao walikuwa wanasafiri kutoka kisiwa cha Yozu kuelekea kisiwa cha Bulyaheke wilayani Sengerema ndipo mtumbwi huo ulipoanza kuingia maji na kusababisha kuzama,” amesema Mutafungwa. 

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Nukta TV

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Nukta TV

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Nukta TV