Mtumbwi waua shabiki wa Yanga, watano hawajulikani

August 6, 2024 5:42 pm · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link

Mwanza. Mtu mmoja amefariki dunia huku wengine watano wakiwa hawajulikani walipo baada ya mtumbwi waliokuwa wanasafiria kuingia maji na kuzama ndani ya Ziwa Victoria usiku wa kuamkia leo wakitoka kusherehekea wiki ya Mwananchi. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Wilbroad Mutafungwa amesema hadi mtumbwi huo unazama uilikuwa na watu 23 ambao ni mashabiki wa timu ya mpira wa miguu ya Yanga ambao walikuwa wanatoka kusherehekea kilele cha Wiki ya Mwananchi wilayani Sengerema.

Mutafungwa amewaambia wanahabari jijini Mwanza kuwa watu wengine 17 waliokuwepo kwenye mtumbwi huo walinusurika na ajali hiyo. 

“Watu hao walikuwa wanasafiri kutoka kisiwa cha Yozu kuelekea kisiwa cha Bulyaheke wilayani Sengerema ndipo mtumbwi huo ulipoanza kuingia maji na kusababisha kuzama,” amesema Mutafungwa. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV