Mrithi wa Maalim Seif nafasi ya makamu wa rais atangazwa Zanzibar

March 1, 2021 10:39 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni mwanachama wa ACT-Wazalendo, Othman Masoud Othman aliyeteuliwa kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar akichukua nafasi ya Maalim Seif Sharif Hamad ambaye alifariki dunia Februari 17 mwaka huu. 
  • Othman aliyewahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar ataapishwa kesho Februari 2, 2021 Ikulu Zanzibar. 

Dar es Salaam. Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi amemteua mwanachama wa ACT-Wazalendo, Othman Masoud Othman kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar akichukua nafasi ya Maalim Seif Sharif Hamad ambaye alifariki dunia Februari 17 mwaka huu. 

Othman aliyewahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar ataapishwa kesho Februari 2, 2021 Ikulu Zanzibar. 

“Baada ya kushauriana na Chama cha ACT-Wazalendo, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dk Hussein Mwinyi amemteua Mheshimiwa Othman Masoud Othman Sharif kuwa Makamu wa kwanza wa rais wa Zanzibar,” imeeleza taarifa ya Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar, Mhandisi Zena Said iliyotolewa leo mchana. 

Kuteuliwa kwa Othman kumekuja baada ya kumalizika kwa kikao kilichowakutanisha vigogo wa ACT-Wazalendo chini ya kiongozi wake mkuu, Zitto Kabwe mwisho mwa wiki kilichofanyika jijini Dar es Salaam kujadili jina la mtu atakayerithi nafasi iliyoachwa na Maalim Seif. 

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 na katika mabadiliko yaliyofanyika mwaka 2010,  inatoa siku 14 kumpata mtu mwingine atakayeziba nafasi ya makamu wa rais baada ya mtu aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo kuondoka au kufariki dunia. 


Soma zaidi:


Othman ambaye kitaaluma ni mwanasheria anakumbkwa kwa kitendo cha kujiuzulua katika nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Uandishi wa Katiba Mpya mwaka 2014 iliyokuwa chini Bunge la Katiba lililokuwa linaongozwa na Hayati Samuel Sitta.

Othman alifikia hatua hiyo baada ya kupendekezwa mambo 17 yenye maslahi kwa Zanzibar yaingizwe ndani ya Katiba iliyopendekezwa na Bunge, lakini yalikatiliwa.

Kujiuzulu kwa kigogo huyo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kulizua taharuki ndani ya Bunge la Katiba na nje kutokana na nafasi aliyokuwa nayo serikalini. 

Kutokana na sintofahamu hiyo, iliwalazimu viongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho Othman alikuwa mwanachama kuazimia kufukuzwa kazi kwa mwanasheria huyo kwa kile walichodai amekisaliti chama.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV