Mkakati wa teknolojia kupambana na Corona wazinduliwa Uswisi

June 2, 2020 7:15 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Mkakati huo wa C-TAP utasaidia upatikanaji wa chanjo, matibabu na teknolojia zingine dhidi ya ugonjwa.
  • Nchi 30 duniani na taasisi za kimataifa likiwemo Shirika Afya Duniani (WHO) wamejiunga katika mkakati huo.

Nchi 30 duniani na taasisi za kimataifa likiwemo Shirika Afya Duniani (WHO) wamejiunga katika mkakati wa kiteknolojia (C-TAP) ili kuharakisha upatikanaji wa chanjo, matibabu na teknolojia zingine dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona.

C-TAP inalenga kuhakikisha chanjo na matibabu ya Corona yanamfikia kila mtu duniani pasipo kujali hali yake. 

Mkakati huo ulipendekezwa kwa mara ya kwanza mwezi Machi na Rais wa Costa Rica Carlos Alvarado ambaye jana amejiunga na Mkurugenzi mkuu wa WHO Dk Tedros Adhanom Ghebreyesus katika uzinduzi rasmi uliofanyika kwa njia ya video mjini Geneva Uswisi.

Dk Tedros ameyakaribisha makampuni na Serikali ambazo zinatengeneza vifaa tiba ili kuchangia muundo wao katika mkakati huu wa tiba. 

“Huu ni wakati ambapo watu wanatakiwa kuweka vipaumbele. Nyenzo za kuzuia, kubaini na kutibu COVID-19 ni masuala muhimu kwa umma ambayo yanahitaji kupatikana kwa wote,” amesema.

C-TAP inatoa fursa ya sehemu moja ambapo patapatikana ujuzi wa kisayansi, takwimu na hati miliki ambavyo vitatumika sawia na jumuiya ya kimataifa katika mapambano ya Corona.


Soma zaidi: 


Kamishina Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet amesema endapo janga la COVID-19  halitodhibitiwa haraka litaendelea kusambaratisha maisha, biashara na chumi na kutuathiri watu wote kwa njia moja au nyingine. 

“Hivyo hebu na tujiunge pamoja kubadilishana takwimu na taarifa, kusongesha mbele uhamishaji wa teknolojia na kupanua wigo wa upatikanaji wa madawa na teknolojia za afya,” amesema Bachelet.

C-TAP inakusudia kuchagiza uvumbuzi wa chanjo, madawa na teknolojia zingine kupitia utafiti ulio wazi wa kisayansi, na kuharakisha uzalishaji kwa kusanya uwezo wa ziada wa wazalishaji.

Hii itasaidia kuhakikisha kuwepo kwa fursa sawa za bidhaa ambazo tayari zipo na mpya za afya za kukabili COVID-19.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV