Mikoa mitatu iliyong’ara matokeo kidato cha sita

July 10, 2021 2:56 pm · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Mkoa wa Singida umeshika nafasi ya kwanza kitaifa.
  • Mikoa ya Lindi na Mara imeingia katika orodha hiyo.

Mwanza. Mkoa wa Singida umetajwa kinara katika motokeo ya mtihani wa kidato cha sita kwa mwaka 2021 yaliyotangazwa leo baada ya kushika nafasi ya kwanza kitaifa.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) Dkt. Charles Msonde akitangaza matokeo hayo leo amesema ufaulu wa jumla umepanda kidogo kwa asilimia 0.11 ambapo mwaka 2020 ulikuwa 99.51 na mwaka huu ufaulu ni asilimia 99.62.

Ufaulu huo ni sawa na ongezeko la asilimia 0.11.

Dk Msonde wakati akitangaza matokeo hayo ametaja mikoa mitatu iliyofanya vizuri kuwa ni Singida ambao umeshika nafsi ya kwanza ukifuatiwa na Lindi huku nafasi ya tatu ikienda kwa Mkoa wa Mara.

Singida ambayo ilikuwa na shule 15 idadi ya watahiniwa 1,674 waliofanya mtihani huo, imepata ubora wa ufaulu wa asilimia 73.91 ikiwa ni kiwango cha juu kuliko mikoa mingine.

Licha ya Singida kushika nafasi ya kwanza, haijafanikiwa kuingiza shule wala mwanafunzi katika orodha ya 10 bora kitaifa.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV