Mfumuko wa bei wang’ang’ania kiwango cha Januari

March 8, 2019 2:09 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ripoti ya mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia Februari 2019 inaeleza kuwa kasi ya kupanda kwa bei za bidhaa na huduma ilibaki asilimia tatu kama ilivyokuwa Januari.

Dar es Salaam. Kasi ya mfumuko wa bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia Februari 2019 imeendelea kubaki kama ilivyokuwa Januari mwaka huu jambo linaloonyesha mwenendo imara wa mabadiliko ya bei katika kipindi hicho.

Taarifa ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imebainisha kuwa mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwaka ulioishia Februari 2019 ulikuwa asilimia tatu ikiwa ni sawa kabisa na kiwango kilichorekodiwa katika mwaka ulioishia Januari 2019.

“Udumavu wa mfumuko wa bei unaonyesha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei ya bidhaa kwa mwaka ulioishia Februari 2019 umebaki kuwa sawa kabisa kama ilivyokuwa Januari 2019,” inaeleza sehemu hiyo ya ripoti ya mfumuko wa bei ya NBS na kuongeza;

“Hata hivyo, faharisi ya bei ilipanda hadi 114.63 Februari 2019 kutoka 111.33 iliyorekodiwa Februari 2018.

Kiwango cha mfumuko wa bei kama hicho pia kilirekodiwa katika mwaka ulioshia Novemba 2018 na ndiyo kidogo kuliko vyote katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
14 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV

Ni changamoto gani zinawakabili vijana wa kitanzania kwa sasa ?

Ni changamoto gani zinawakabili vijana wa kitanzania kwa sasa ?

Nukta TV

Akili Unde (AI) ni suluhu ya habari za uzushi ?

Akili Unde (AI) ni suluhu ya habari za uzushi ?

Nukta TV