Mfumuko wa bei za bidhaa, huduma wapaa Tanzania

February 9, 2023 1:56 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  •  Umeongezeka hadi asilimia 4.9 mwaka ulioishia Januari 2023 kutoka asilimia 4.8 kwa mwaka ulioishia Disemba 2022. 

Dar es Salaam. Kasi ya mfumuko wa bei muhimu za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia Januari 2023 umeongezeka hadi asilimia 4.9 kutoka asilimia 4.8 kwa mwaka ulioishia Disemba 2022. 

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) katika taarifa yake iliyotolewa leo Februari 9, 2023 imesema kuongezeka kwa mfumuko kwa mwaka ulioishia Januari 2023 kumechangiwa na kuongezeka kwa mfumuko wa bei kwa baadhi ya bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula.

Baadhi ya bidhaa za vyakula ambazo mfumuko wake wa bei umeongezeka ni ngano kutoka asilimia 6 hadi asilimia 7.7, unga wa mtama (kutoka asilimia 1 hadi asilimia 3.9), samaki (kutoka asilimia 4.2 hadi asilimia 4.3) na matunda kutoka asilimia 1.9 hadi asilimia 5.5.

Bei ya mbogamboga imeongezeka kutoka asilimia 3.6 hadi asilimia 5.2, viazi vitamu (kutoka asilimia 3.9 hadi asilimia 5.3),  choroko (kutoka asilimia 1.3 hadi asilimia 5.6) na kunde kutoka asilimia 8.7 hadi asilimia 13.9.


Zinazohusiana


Baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizoonyesha kuongezeka kwa mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia Januari 2023 ikilinganishwa na mwaka ulioishia Disemba 2022 ni pamoja na nguo za wanawake kutoka asilimia 2.6 hadi asilimia 2.7, viatu vya wanawake (kutoka asilimia 3.4 hadi asilimia 3.5) na vifaa muhimu kwa matumizi ya nyumbani kutoka asilimia 2.2 hadi asilimia 3.5.

Dizeli imeongezeka kutoka asilimia 27.4 hadi asilimia 33.1, petroli (kutoka asilimia 3.7 hadi asilimia 4.7), ada za shule (kutoka asilimia 0.7 hadi asilimia 2.9) na huduma ya malazi kwenye hoteli na nyumba za kulala wageni kutoka asilimia 0.9 hadi asilimia 3.8.

“Mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwaka ulioishia mwezi Januari 2023 umeongezeka hadi asilimia 9.9 kutoka asilimia 9.7 kwa mwaka ulioishia Disemba 2022,” imeeleza NBS katika taarifa hiyo.

Mfumuko wa Bei ambao haujumuishi bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa  umeongezeka kidogo hadi asilimia 3 kutoka asilimia 2.9.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.