Maumivu kwa wawekezaji wa kampuni ya bia soko la hisa Dar

May 24, 2019 4:29 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

EABL ndiyo kampuni iliyofanya vibaya zaidi leo sokoni huku nyingi zikibaki katika viwango vilivyokuwepo jana zikiwemo Vodacom, benki ya CRDB, DCB na NMB. Picha|Mtandao.


  • Hisa za kampuni hiyo ya bia ya Afrika Mashariki (EABL) katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) zimeshuka kwa asilimia 0.85. 
  • Wawekezaji wake wamepoteza Sh40 kwa kila hisa moja leo sokoni.
  • Kampuni ya habari ya NMG na Acacia wako kicheko tu.

Dar es Salaam. Wawekezaji wa kampuni ya Bia ya Afrika Mashariki (EABL) katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) leo wamepoteza Sh40 kwa kila hisa ya moja baada ya thamani ya hisa za kampuni hiyo kushuka kwa asilimia 0.85 kutoka kiwango cha jana Mei 23, 2019.

Ripoti ya soko ya siku ya DSE ya Mei 24 inaonyesha kuwa hadi soko linafungwa thamani ya hisa moja ya EABL ilikuwa ni Sh4,640 kutoka Sh4,680 iliyorekodiwa jana. 

Licha ya thamani ya hisa za kampuni hiyo kushuka, haikufanikiwa kuuza hata hisa moja leo.

Wakati wawekezaji wa EABL wakiugulia maumivu leo, wenzao wa kampuni ya Kenya Airways(KA) watalala na kicheko baada ya thamani ya hisa za kampuni hiyo kupanda kwa asilimia 6.67 kutoka Sh75 kwa hisa moja iliyorekodiwa jana wakati soko linafungwa hadi Sh80 leo hii jioni. 

Kampuni nyingine ambazo thamani ya hisa zake imeongezeka ni kampuni ya Habari ya NMG (National Media Group) ambayo imepanda kwa asilimia 3.33 na  Acacia (asilimia 1.33).


Zinazohusiana: 


EABL ndiyo kampuni iliyofanya vibaya zaidi leo sokoni huku nyingi zikibaki katika viwango vilivyokuwepo jana zikiwemo Vodacom, benki ya CRDB, DCB na NMB.

Hata hivyo, benki ya CRDB  imeongoza kwa  kuuza kiwango kikubwa cha hisa sokoni leo kwa kuuza hisa 64,355 sawa na asilimia 66.8 ya hisa zote zilizouzwa ikifuatiwa na TBL (asilimia 27.9) na Vodacom (asilimia 5.2). 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Sep, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Sep, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴 LIVE: WABUNGE WAKIMCHAPA MASWALI MAZITO WAZIRI MKUU BUNGENI

🔴 LIVE: WABUNGE WAKIMCHAPA MASWALI MAZITO WAZIRI MKUU BUNGENI

Nukta TV

CEO, TAB Group: Africa Agri Expo 2026 inakwenda kufungua fursa kimataifa, kilimo cha Tanzania

CEO, TAB Group: Africa Agri Expo 2026 inakwenda kufungua fursa kimataifa, kilimo cha Tanzania

Nukta TV

TANTRADE: Tumieni vifungashio vya "Made in Tanzania"

TANTRADE: Tumieni vifungashio vya "Made in Tanzania"

Nukta TV