Mambo yatakayosaidia kukuza uchumi wa Tanzania wakati wa Uviko-19
Dar es salaam. Wakati janga la corona likiendelea kutikisa dunia, nchi nyingi ikiwemo Tanzania zimeathirika kiuchumi kutokana na kupungua kwa shughuli za biashara na uzalishaji.
Mathalan, uchumi wa Tanzania ulikuwa kwa asilimia 4.8 mwaka 2020 ikilinganishwa na asilimia 7 mwaka juzi, kwa mujibu Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Licha ya athari za ugonjwa huo katika sekta ya uchumi nchini, kuna nafasi ya kukuza sekta hiyo endapo nchi itachukua hatua mbalimbali.
Kuongeza vita dhidi ya Uviko-19, itasaidia kuokoa maisha na kulinda nguvu kazi lakini kutaongezeka ajira na kuimarika kwa sekta binafsi hivyo kuinua tena upya uchumi.
