Mambo yatakayosaidia kampuni chipukizi wakati wa Uviko-19
- Ni pamoja na punguzo la kodi kwa kampuni hizo.
- Utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu.
Dar es Salaam. Kutokana na janga la Uviko-19 kuathiri utendaji wa kampuni zinazochipukia (startups) nchini, hatua muhimu zinahitajika kufanyika ili kuzisaidia kampuni hizo kukua na kuimarika tena.
Hatua hizo ni pamoja na utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa kampuni chipukizi ili ziweze kupata mitaji ya kuendeleza biashara zao wakati wa Uviko-19.
Vilevile, kupunguzwa kwa kodi ili kuzipa uhueni kampuni hizo kutokana na mwenendo usioridhisha wa biashara.
