Malengo: Ngazi ya kukufikisha katika ndoto zako

May 3, 2021 11:57 am · Neema
Share
Tweet
Copy Link
  • Mipango iko kwenye kila jambo unalolifanya hata kama ni dogo kiasi gani.
  • Anza leo kupanga kuhusu mustakabali wa baadaye wa maisha yako.

Dar es Salaam. Kupanga ni kuchagua. Na uchaguzi unategemea anayepanga anataka nini kwenye maisha yake. Mipango iko kwenye kila jambo unalolifanya hata kama ni dogo kiasi gani. 

Mathalan, unapotaka kutoka nyumbani asubuhi ni lazima utajipanga utoke vipi kwa maana utachagua nguo nzuri ambayo unaamini itakufaa kwa siku hiyo. Hapo umepanga mipango.

Hata wewe kijana unayesoma makala hii, unatakiwa kuwa na mipango iliyojitosheleza kuhusu maisha yako. Usisubiri kufika ngazi fulani ya maisha. Anza leo kupanga kuhusu mustakabali wa baadaye wa maisha yako.

Labda nikuambie tu, mipango siyo kitu cha ajabu ambacho kinatakiwa kufanya na watu fulani. Ni suala la kila mtu. Mipango ni  maamuzi ya makusudi  ambayo mtu anajiwekea ili kutimiza  jambo akitarajia kupata matokeo fulani.

Kuna ulazima wa kuwa na mipango? Ndiyo kwa sababu usipojipanga watakupanga watu wengine kwenye maisha yako. Ukiwa na mipango una nafasi kubwa ya kuboresha maisha yako:

Ni ramani ya kukuongoza

Ukiwa na mipango yako binafsi ni kama umejitengenezea ramani yako mwenyewe ambayo unatakiwa kupita kufika unakokwenda.

Hii itakusaidia kuepuka vitu visivyo na maana kwenye maisha na kukufanya utazame mambo ya msingi yenye manufaa kwenye maisha. Ramani itakulazimisha kutumia muda na rasilimali fedha vizuri. 

                                

Hutayumbishwa na chochote

Watu wenye mipango hawayumbishwi na chochote kwenye jamii kwa sababu wanatambua nafasi waliyonayo. Utakuja kila namna ya upepo wa mitindo na mifumo isiyo rafiki, wao watabaki kwenye msimamo walionao.

Kuna mambo yanakuyumbisha kwenye jamii? Huna mipango. Anza kupangilia mambo yako ili usipangwe na watu wengine. 


Soma zaidi: 


Utajenga uaminifu

Miapngo inajenga uaminifu kwa wanaokuzuguka. Matokeo mazuri kwenye kazi au biashara yanayotokana na mipango ambayo itakufanya uaminiwe na watu unaofanya nao kazi. 

Unataka kuanza leo? Basi hujachelewa tafakari kuhusu maisha yako na pangilia kila jambo unalofanya kwenye maisha yako.   

Hadi wakati  mwingine tukutane tena hapa hapa katika kipindi chako cha mimi na wewe tuzungumze zaidi.  

Neema Simbo ni mjasiriamali na mwandishi wa vitabu. Unaweza kuwasiliana naye kwa namba ya simu: +255 763 009 933 au Instagram: @eden_kush

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Nukta TV

Sakata bei ya mafuta kupanda latua BoT, Naibu Gavana atoa ufafanuzi

Sakata bei ya mafuta kupanda latua BoT, Naibu Gavana atoa ufafanuzi

Nukta TV

BoT yabakiza Riba ya Benki Kuu 5.75% kudhibiti mfumuko wa bei

BoT yabakiza Riba ya Benki Kuu 5.75% kudhibiti mfumuko wa bei

Nukta TV