Makosa ya kuepuka wakati wa kuvaa barakoa

August 23, 2021 1:59 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na kuvaa barakoa chini ya kidevu au kutokuziba pua au mdomo.
  • Barakoa inatakiwa kutumika vizuri ili kumkinga mtumiaji wake na maambukizi.

Dar es Salaam. Uvaaji wa barakoa ni kati ya vitu vinavyoshauriwa na mamlaka za afya kama hatua za kuchukuliwa ili kukomesha usambaaji wa virusi vya Corona.

Hata hivyo, kutokana na baadhi ya watu kukosa elimu, wanajikuta wakitumia barakoa huku wakifanya makosa mbalimbali ya uvaaji kama kuivaa barakoa bila kufunika pua, kuning’iniza barakoa kwenye sikio moja, na kuivaa chini ya kidevu.

Hali hiyo inaweza kusababisha mtu kupata maambukizi ya ugonjwa wa Corona na hivyo matumizi yake ya barakoa yanakuwa hayana tija katika vita ya kupambana na kusambaa kwa virusi vya Corona.

Tazama video hii kona makosa ambayo baadhi ya watu wanayafanya katika matumizi ya barakoa.

                        

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW