Majaliwa mgeni rasmi maombi ya kitaifa dhidi ya Corona

April 21, 2020 5:38 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Yatakayofanyika kesho katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
  •  Maombi hayo yameandaliwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Viongozi wa madhehebu ya Dini nchini. 

Dar es Salaam. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa atakuwa mgeni rasmi katika maombi ya kitaifa ya kuombea nchi dhidi ya janga la Corona (#COVIDー19) yatakayofanyika kesho katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

Maombi hayo yameandaliwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Viongozi wa madhehebu ya Dini nchini.  

Wizara ya afya katika taarifa yake iliyotolewa leo imesema maombi hayo  yatakayoongozwa na viongozi wakuu wa  madhehebu ya dini nchini, yatafanyika kesho Aprili 22, 2020 katika Viwanja vya Karimjee.

“Hatua hii ni utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa viongozi wa dini na Serikali uliofanyika tarehe 9 Aprili, 2020 Jijini Dar Es Salaam kuwa yafanyike maombi ya kitaifa yanayojumuisha madhehebu yote nchini kuomba dhidi maambukizi ya Corona,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo.


Zinazohusiana


Aidha,maombi haya ni mwendelezo wa maombi ya siku tatu mfululizo yaliyotangazwa na Mhe. Rais John Magufuli kuanzia Aprili 17-19, 2020.

“Viongozi wachache watahudhuria maombi haya kuwakilisha wananchi ikiwa ni katika hali ya kuchukua tahadhari ya maambukizi hivyo, wananchi mnasisitizwa kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya Corona na kufuatilia maombi haya mkiwa katika maeneo yenu kupitia vyombo mbalimbali vya habari,” inaeleza taarifa hiyo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Nukta TV

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Nukta TV

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Nukta TV