Magufuli awatoa hofu watalii wanaotembelea Tanzania

July 20, 2020 10:02 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Amesema Corona iko mbali na Tanzania, watalii wanaweza kuingia bila wasiwasi.
  • Aitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kuitangaza Tanzania kimataifa. 

Dar es Salaam. Rais John Magufuli amewatoa hofu watalii wanaokuja Tanzania kwa sababu nchi iko salama dhidi ya ugonjwa wa Corona, huku akiitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kuendelea kuitangaza nchi kimataifa.

Dk Magufuli aliyekuwa akizungumza leo (Julai 20, 2020) jijini Dodoma wakati akiwaapisha viongozi walioteuliwa wiki iliyopita akiwemo Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki amesema kwa sasa Corona iko mbali na Tanzania, watalii wanaweza kuja bila wasiwasi. 

“Corona iko mbali kule, ilimalizwa kabisa. Tuliamua kumuomba Mungu, tukamtanguliza Mungu na Mungu akatusikia. Kila mtalii atakayekuwa anakuja atakuja ataangalia wanyama wake na atarudi akiwa salama,”  amesema Dk Magufuli.


Zinazohusiana


Amesema ameshuhudia watalii wakiendelea kuingia nchini kwa wingi jambo linalodhihirisha kuwa kwa sasa Tanzania iko salama.

“Nimeanza kuona watalii wanakuja wengi na ndege zinaleta watalii wengi, watu wameshaanza kuangalia na kuuona ukweli kwamba hapa Tanzania tuko salama,” amesema Dk Magufuli.

Aidha, ameiagiza wizara ya Maliasili na Utalii kuendelea kuitangaza Tanzania kimataifa ili kuvutia watalii wengi zaidi.

Kwa viongozi wengine walioteuliwa, Rais Magufuli amewasisitiza kuendelea kushirikiana kwa karibu na viongozi katika maeneo waliyopangiwa kazi ili kuwaletea wananchi maendeleo.

“Ni bahati nzuri tumeingia kwenye uchumi wa kati. Ni matumiani yangu mtauendeleza huo uchumi wa kati mpaka ukawe uchumi wa juu zaidi. Ni matumaini yangu mtaweza kufanya kazi nzuri,”  ameyasema Rais Magufuli. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV