Madiwani Arusha, Ilemela wabadilishana uzoefu miradi ya maendeleo

January 17, 2023 12:41 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Wakutana Mwanza kujifunza mkoa huo unavyotekeleza miradi ya kimkakati.

Mwanza. Timu ya madiwani na wataalam kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Arusha imefanya ziara katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela yenye lengo la  kujifunza namna halmashauri hiyo ilivyoweza kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo na kutoa matokeo chanya.

Mradi mmojawapo ambao umevutia na kuwa chao ya wao kutembelea ni stendi ya mabasi na maegesho ya malori uliopo Nyamh’ongolo mkoani Mwanza.

Akizungumza baada ya kutembelea mradi huo uliogharimu zaidi ya Sh26 bilioni zikiwemo gharama za maegesho ya malori na gharama za mshauri, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha Ojung’u Salekwa amepongeza juhudi zilizofanywa na timu ya Ilemela kuhakikisha wanakamilisha kazi hiyo ya ujenzi wa stendi ya kisasa.

“Kwa hiki kinachoonekana ni dhahiri kuwa Ilemela kuna ushirikiano mzuri kati ya madiwani na wataalam, tumefurahishwa na kazi iliyofanyika hapa na tutaiga mfano wenu,” amesema Salekwa.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela, Renatus Mulinga amepongeza uamuzi wa madiwani na wataalam hao kutembelea Ilemela kwa ajili ya kujifunza na kuelezaa kuwa hilo ni jambo la kutia moyo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Mhandisi Modest Apolinary, amesema kazi ya ujenzi wa stendi hiyo imefanywa kwa ushirikiano mkubwa wa madiwani na wataalamu wa halmashauri hiyo.

“Tuna kauli mbiu yetu kuwa Ilemela ni yetu sote tushirikiane kuijenga hivyo kila mmoja kwa nafasi yake anapaswa kuwajibika kuhakikisha tunakamilisha miradi yote tuliyojiwekea,” amesema Apolinary.

Amesema kwa sasa halmashauri hiyo imeendelea kuibua vyanzo mbalimbali vya mapato pamoja na kuboresha usimamizi wa vilivyopo.

Mtaalam wa miradi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela James Wembe, amesema ni vizuri kushirikisha wataalam washauri wa ndani na nje ya halmashauri kutoa mawazo yao katika masuala ya miradi inayotekelezwa eneo husika.

“Zipo hatua za kufuata katika kufanikisha miradi mikubwa kama hii, kuanzia mpango (planning), utekelezaji (Implementations) na kazi yenyewe (operations),” amesema Wembe.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV