Madhara yatakayokupata usipotibu ugonjwa mapema

November 28, 2020 6:16 am · Joshua
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na kutumia gharama kubwa za matibabu.
  • Pia ugonjwa kukosa tiba kabisa na hatimaye kifo.
  • Ukipata maumivu ya mwili, nenda hospitali kapate tiba. 

Nabaki na tafakuri nzito, wakati nikipitia baadhi ya taarifa za wagonjwa wangu kwenye mafaili kadhaa katika kabati ya kutunzia kumbukumbu za wagonjwa katika kituo cha kazi.

Tafakuru hiyo inakuja kwa sababu nakutana na rekodi za baadhi ya wagonjwa zisizofurahisha hasa za wagonjwa ambao nina ukaribu nao. 

Taarifa zao ambazo zipo kwenye mafaili ya hospitali hazifurahishi. Kimsingi hakuna kinachofurahisha kuhusu ugonjwa, lakini vipo vile ambavyo husikitisha zaidi kuliko vingine. 

Rekodi za mafaili yao zinaonyesha wamefikia hatua mbaya za ugonjwa na wako katika hatari kugharimika zaidi kupata tiba. 

Changamoto kubwa ya kiafya inyowapata watu ni kufika hospitali katika hatua za mwisho au sugu za ugonjwa. Katika hatua hizi, ugonjwa unakua umefika katika hatua mbaya isiyoweza kurejesha hali ya kawaida.

Wakati mwingine mgonjwa hutumia gharama kubwa au kupoteza baadhi ya viungo vya mwili na hata kufariki dunia.


Zinazohusiana:


Utambuzi wa dalili za ugonjwa unapofanyika mapema huwezesha utolewaji wa tiba husika mapema, kwa namna hiyo humsaidia mgonjwa kupona na kurudia hali ya kawaida haraka iwezekanavyo. 

Unapohisi dalili za ugonjwa ama unapojisikia vibaya na hali hiyo ikajirudia mara kadhaa, ni vyema kufika hospitali na kuonana na mtoa tiba ili uweze kuhudumiwa ipasavyo. 

Matumizi ya dawa za kuondoa maumivu mara kwa mara kwa tatizo ambalo halijatambuliwa na mtaalamu ni hatari. Maumivu ni ishara ambayo mwili hutumia kutoa taarifa za hitilafu sehemu fulani. 

Usipuuzie maumivu, uvimbe au hali yoyote isiyo ya kawaida kwa muda mrefu. Muone muhudumu wa afya akuhudumie.

Nipo!

Dk Joshua Lameck Sultan ambaye kitaaluma ni daktari wa mafunzo ya mazoezi tiba ni Mshauri katika taasisi ya Nakua na Taifa Langu (NTL) na Mkurugenzi wa Indigo Afya. Hufanya semina mbalimbali kuhusu masuala ya afya akijikita katika magonjwa yasiyoambukiza (NCD) pamoja na yale yanayoendana na mtindo maisha. Anapatikana kwa namba: +255 789 311 481, Baruapepe: joshualameck9@gmail.com.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV