Live: Safari ya mwisho ya Hayati John Magufuli
Dar es Salaam. Baada ya kuishi miaka zaidi ya 61 ulimwenguni, John Magufuli, Rais wa tano wa Tanzania atakuwa akipumzishwa katika makazi yake ya milele katika makaburi ya familia huko Chato mkoani Geita leo alasiri.
Hayati Rais Magufuli alifariki dunia Machi 17 mwaka huu jijini Dar es Salaam katika hospitali ya Mzena alipokuwa akipatiwa matibabu ya maradhi ya moyo.
Misa ya kumuombea Hayati Rais Magufuli, inayofanyika katika kiwanja cha Magufuli mjini Chato, inaongozwa na Askofu Mkuu, Gervas Nyaisonga, Rais wa Baraza la Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC).
Latest