Kwanini uchague filamu ya “Star Wars” msimu wa sikukuu

December 20, 2019 4:57 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Inaanza kuonyeshwa rasmi leo (Disemba 20, 2019).
  • Ni mfululizo wa sehemu ya sita ya filamu za Star Wars. 
  • Imejaa mafunzo lukuki yatakayokujenga mwisho wa mwaka 2019.

Dar es Salaam. Unaonaje ukiachana na makaratasi pamoja na skrini ndogo ya kompyuta yako na badala yake kuchagua skrini kubwa ya sinema kufurahia wikiendi yako?

Ndiyo, unastahili mapumziko mazuri ya mwisho wa mwaka ili kujipanga na mwaka ujao yaani 2020 ambao utaanza ndani ya siku 11 zijazo.

Furahia filamu ya “Star Wars” na nyinginezo zilizoingia sokoni katika msimu huu wa sikukuu za mwisho wa mwaka katika kumbi za sinema za Century Cinemax zilizopo Tanzania:

Kwanini Star wars?

Baada ya mapigano ya Crait, Kylo Ren (Daisy Ridley) anaanza safari yake kuelekea sayari ya Exegol ambapo anakutana na Palpatine ambaye anafunguka kuwa chanzo cha Snoke ambaye alikuwa ni kibaraka aliyedhamiria kumrubuni Ren ageukie upande wa “dark side” (moja ya majeshi kwenye ulimwengu wa Star Wars).

Ni kipigo juu ya kipigo, muungano baada ya muungano huku mafunzo yakiwa ni umuhimu wa kuwa na watu wa karibu ambao wapo tayari kusafiri maili moja na wewe.

Shuhudia meli za vita za angani, maji yaliyozidi kina na zaidi, unaachaje kuona jinsi “Ightsaber” (silaha za kivita za wapiganaji) zinavyoendelea kuchukua nafasi?


Zinazohusiana


Usiache kuenda na mwanao au familia kutazama filamu hii iliyogharimu takribani Sh729.4 bilioni ambayo inawakutanisha manguli kama John Boyega (Finn), Billy Williams (Lando Calris) ambaye alitisha kwenye filamu ya “Bat Man” na “Undercover Brother”.

Utaweza kuiona filamu hii imeongozwa na Jeffrey Abrams, kiongozi wa filamu zaidi ya 40 zikiwemo za “Mission Impossible” na “Overload” kwa Sh5000 siku ya Alhamis na Sh10,000 siku za wikiendi.

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...