Kicheko: Bei ya petroli, dizeli ikishuka kwa mwezi Septemba Tanzania

September 3, 2025 9:57 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Bei ya petroli yafikia Sh2,807 na dizeli 2,754

Arusha. Kwa watumiaji wa mafuta ya petroli na dizeli huenda wakauanza mwezi Septemba kwa kicheko baada ya bei ya nishati hiyo kushuka kwa sh26 na Sh23 kwa lita mtawalia.

Ahueni hii inakuja ikiwa ni mwezi mmoja baada ya dizeli kupaa kiduchu kwa kwa Sh 10  hali iliyofanya watumiaji kutoboa mifuko yao kujipatia bidhaa hiyo.

Taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji Tanzania (Ewura) leo Septemba 3, 2025 inabainisha kuwa bei ya rejareja ya petroli  ni Sh 2,807 huku dizeli ikiuzwa kwa Sh2,754.

Bei hizo za reja reja kupitia bandari ya Dar es Salaam zimeshuka kutoka Sh2,843 kwa petroli na Sh2,777 kwa dizeli zilizokuwa zinatumika mwezi uliopita.

Kwa mujibu wa Ewura bei hio zimeshuka kutokana na kuongezeka kwa gharama za mafuta yaliyosafishwa (FOB) katika soko la Uarabuni.

“Katika bei kikomo kwa Septemba 2025, bei za mafuta katika soko la dunia zimepungua kwa asilimia 0.2 kwa mafuta ya petroli, asilimia 5.5 kwa mafuta ya dizeli na asilimia 3.5 kwa mafuta ya taa,” imesema taarifa ya Ewura.

Wakati bei hiyo ikishuka, gharama za kuagiza mafuta (premiums) katika Bandari ya Dar es salaam zimeongezeka kwa wastani wa asilimia 20.73 kwa mafuta ya petroli, asilimia 7.75 kwa mafuta ya dizeli na asilimia 2.62 kwa mafuta ya taa.

Pamoja na ahueni hiyo  bado wakazi wa Kyerwa (Ruberwa) ndiyo wanaonunua mafuta hayo kwa bei ya juu zaidi ya Sh3,079 kwa petroli na Sh3,027 kwa dizeli ikiwa ni Wastani wa Sh200 zaidi ya bei inayotumiwa na wakazi wa jiji la Dar es Salaam.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV