Bei ya petroli Dizeli yashuka kwa mara ya pili mfululizo Tanzania

October 1, 2025 12:01 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Petroli yauzwa Sh2,752 na dizeli Sh2,704.
  • Bei ya nishati hizo katika soko la dunia na gharama za uagizaji zapaa.

Arusha. Mwezi Oktoba umeanza kwa kicheko kwa watumiaji wa mafuta ya petroli na dizeli baada ya bei ya nishati hiyo kushuka kwa mara ya pili mfululizo.

Taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji Tanzania (Ewura) leo Oktoba1 , 2025 inabainisha kuwa bei ya rejareja ya petroli  ni Sh 2,752 huku dizeli ikiuzwa kwa Sh2,704.

Kutokana na bei hizo, petroli imeshuka kwa Sh55 kutoka Sh2,807 iliyokua ikitumika mwezi Septemba na dizeli imeshuka kwa Sh50 kutoka Sh2,754 iliyotumika mwezi uliopita.

Ahueni hii inakuja ikiwa ni miezi miwili baada ya dizeli kupaa kiduchu kwa kwa Sh 10  hali iliyofanya watumiaji kutoboa mifuko yao kujipatia bidhaa hiyo.

Licha ya kushuka kwa bei ya mafuta nchini Tanzania, EWURA inasema bei ya nishati hizo katika soko la dunia na gharama za uagizaji kupitia bandari za Dar es Salaam, Mtwara na Tanga zimeongezeka.

“Bei za bidhaa za mafuta ya petroli hapa nchini zinazingatia gharama za mafuta yaliyosafishwa (FOB) katika soko la nchi za Kiarabu. Katika bei kikomo kwa Oktoba 2025, bei za mafuta katika soko la dunia zimeongezeka kwa asilimia 2.80 kwa mafuta ya petroli, asilimia 3.65 kwa mafuta ya dizeli na asilimia 3.57 kwa mafuta ya taa.” imesema taarifa ya EWURA.

Kwa upande wa gharama za  uagizaji mafuta (premiums) katika Bandari ya Dar es Salaam zimepungua kwa wastani wa asilimia 1.95 kwa mafuta ya petroli, zimeongezeka kwa asilimia 2.39 kwa mafuta ya dizeli na hakuna mabadiliko kwa mafuta ya taa.

Katika Bandari ya Tanga zimeongezeka kwa asilimia 6.38 kwa mafuta ya petroli na dizeli na katika Bandari ya Mtwara zimeongezeka kwa asilimia 0.49 kwa mafuta ya petroli na hakuna mabadiliko kwa mafuta ya dizeli.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
25 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

Nukta TV

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

Nukta TV

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

Nukta TV