Jinsi ya kupika samaki aina ya Nguruka 

January 29, 2025 6:59 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Nguruka anaweza kuchomwa na kusindikizwa na ugali pamoja na kachumbari.
  • Pia unaweza kuandaa rosti ambalo unaweza ukala na wali au chakula kingine.

Nguruka ani miongoni mwa aina za samaki zilizojizolea umaarufu katika mkoa wa Morogoro ambao wenyeji wake wanauita ‘mji kasoro bahari’.

Kwa wageni mkoani humo wanaweza kudhani  jina la samaki huyo ni kirefu cha samaki nguru ambaye mara nyingi huuzwa kwa vipande katika miji na maeneo ya pwani.

La hasha, nguruka ni tofauti na samaki nguru na utofauti wake upo kwenye maandalizi hadi muonekano wa nje ambapo samaki nguruka huwa wadogo wadogo wanaoandaliwa kwa mafuta ya mawese na chumvi nyingi wakati samaki aina ya nguru mara nyingi huuzwa wakiwa wamekatwa vipande.

Wenyeji wa Morogoro wanafahamu utamu wa samaki huyo hususan akichomwa na kusindikizwa na ugali pamoja na kachumbari.

Mbali na aina hiyo iliyozoleka jikopoint inakuletea maandalizi rahisi ya rosti la nguruka unaloweza kula pamoja na wali, chapati au aina nyingine ya msosi.

Rosti la nguruka hunoga kwa wali hususani ukiwa wali wa nazi. Iyawa/Instagram. cookhouse

Maandalizi

Kwa kuwa nguruka ni samaki mwenye chumvi hivyo hatua ya kwanza ni kuloweka katika maji ya moto kwa dakika kadhaa ili kupunguza chumvi iliyopo kisha unaweza kumtoa na kumuweka katika chombo kisafi kwa ajili ya mapishi.

Hatua hiyo pia itakusaidia kupunguza mafuta ya mawese yanayotumika kuhifadhia samaki huyo kama hupendelei.

Baada ya hapo utaendelea na maandalizi ya kawaida ambayo ni kumenya nyanya, vitunguu,nyanya chungu, kusaga karoti na kukuna nazi ili kutoa matui mawili.

Anza mapishi yako kwa kuwasha jiko, bandika sufuria na ikipata moto uweke mafuta kiasi ikifuatiwa na vitunguu ambavyo utavipika kwa dakika moja au mbili vikifuatiwa na nyanya chungu.

Hatua inayofuata ni kuweka nyanya na kuzifunika mpaka ziive kisha utaweka tui la pili utakaloliacha jikoni mpaka lichemke ikifuatiwa na nguruka na baadae tui zito la kwanza.

Ukifika hatua hii acha tui lichemke kisha uongeze chumvi (kama iliyopo haitoshi) pilipili hoho, karoti zilizosagwa na pilipili kama unatumia.

Acha vyote vichemke na kuiva vizuri na ukiridhika na kiwango cha mchuzi kilichobakia mboga yako itakuwa tayari kwa kuliwa.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV