Jinsi unavyoweza kupika maini rosti

September 29, 2022 10:24 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Mboga hii inafaa kuliwa na wali, ugali, chapati au ndizi.
  • Inafaa kuliwa wakati wowote iwe mchana au jioni.

Iwe wakati wa mchana au jioni suala la kuchagua mboga halijawahi kumuacha mtu salama, lazima uumize kichwa kujua mboga itakayosukuma mlo wako wa siku husika.

Kama kawaida leo nimekusogezea mapishi rahisi ya rosti ya maini ya ng’ombe unayoweza kula na wali, ugali, ndizi au hata chapati.

Basi tusogee jikoni tupike hii mboga yenye ladha ya kipekee, na kwa hakika mpaka umalize kuipika utakuwa umeshapata chakula ambacho kitaisindikiza mboga hii kwenye meza yako ya msosi.

Maandalizi

Osha maini na uyakate kate vipande kiasi, kicha uchuje maji na uyaweke kwenye chombo kisafi.

Ukimaliza andaa nyanya, karoti, hoho kitunguu kwa kuosha na kukata kata saizi uipendayo, kisha twanga tangawizi na kitunguu saumu mpaka vitakapolainika.

Andaa sufuria ya kupikia, ibandike jikoni na uanze kwa kuweka mafuta na vitunguu ulivyokwisha kukata kata kisha ukoroge mpaka vikiwa rangi ya kahawia.

Baada ya hapo ongeza kitunguu swaumu na tangawizi na ukoroge kwa dakika moja uache viive kisha ongeza maini na uache yaive.

Kila baada ya dakika 3 uwe unageuza maini yako ili yasiungue hadi maji yakauke na kuonyesha dalili za kuiva.

Ongeza nyanya ulizokata kata kwenye sufuria unayopikia maini yako na ufunike kwa dakika 5 ili nyanya ziive.

Nyanya zikishaiva koroga vizuri na uongeze vijiko viwili vya nyanya ya kusaga kisha hoho na karoti na kiasi kidogo cha maji kisha uache jikoni kwa dakika tatu.

Baada ya dakika tatu ongeza chumvi na ndimu kipande kimoja, ukihakikisha rosti yako imekuwa nzito vya kutosha unaweza kuepua na pishi lako litakuwa tayari.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
20 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Prof. Mbalawa, Waziri Misri wavutana, makubaliano ujenzi Bandari ya Bagamoyo

Prof. Mbalawa, Waziri Misri wavutana, makubaliano ujenzi Bandari ya Bagamoyo

Nukta TV

Rais Samia: Nchi za Afrika zinaweza, bila ushiriki wa mataifa ya nje

Rais Samia: Nchi za Afrika zinaweza, bila ushiriki wa mataifa ya nje

Nukta TV

Mfahamu ‘African Goose’ bata mwenye kilo 14 anayeuzwa Sh2 milioni

Mfahamu ‘African Goose’ bata mwenye kilo 14 anayeuzwa Sh2 milioni

Nukta TV