Jinsi ya kuandaa futari ya mihogo na samaki

March 22, 2024 11:42 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Hii  ni namna mpya ya kuandaa futari ya mihogo ya nazi.
  • Utahitaji Oven ya umeme au jiko la mkaa kwa ajili ya kuoka samaki.

Ni kawaida kwa watu waliofunga kufungulia kwa kupata kifungua kinywa kinachoambatana na aina mbalimbali za vyakula na vinywaji. 

Baadhi ya watu huita kifungua kinywa hicho futari hususan waumini wa dini ya kiislamu ambao katika kipindi hiki wapo kwenye mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Msimu huu ndipo ambapo utakuta mapishi ya aina mbalimbali za futari ikiwemo ya mihogo na samaki ambayo ni miongoni mwa futari maarufu.

Licha ya umaarufu huo Jikopoint imekusogezea namna mpya ya kuandaa pishi hili bila jasho huku ukijihakikishia kupata ladha tamu itakayofaa kwa ajili ya kutumiwa na watu wa rika zote.

Maandalizi 

Tuanze maandalizi ya futari kwa kumenya mihogo, ambapo utahitajika kutoa maganda ya nje, kukata vipande vidogo vidogo na baadae kuiosha.

Endelea kwa kukuna nazi kwa kutumia kibao cha mbuzi au kusaga na  blenda kisha chuja na utengnisha tui jepesi na lile zito. 

Unaweza ukatengeneza  matui mawili au zaidi kulingana na wingi wa nazi na ikiwa unatumia nazi za pakti basi hakuna haja ya kutenganisha matui.

Baada ya hapo washa jiko na ubandike mihogo yako jikoni weka tui la pili, vitunguu na chumvi kiasi, acha ichemke hadi pale tui likikaribia kukauka ndipo uongeze tui la kwanza na uache jikoni adi pale mihogo itakapoiva.

Ikiwa unataka mihogo yako iive bila kuwa na mchuzi mwingi basi utaweka tui la nazi kidogo kidogo mpaka pale utakaporidhishwa na kiwango cha rojo kilichopo.

Ukimaliza kuandaa mihogo endelea na maandalizi ya samaki ambapo utamsafisha kisha kumuwekea viungo kadri unavyopendelea.

Baadhi ya viungo unavyoweza kutumiani pamoja na soya sosi, fish masala, manjano, pilipili manga, mdalasini, kitunguu swaumu, tangawizi, mafuta ya kupikia na pilipili ya unga kiasi kama unapendelea.

Changanya viungo vyote na upake samaki wako kisha uwaaache viungo viingie kwa nusu saa au saa1.

Bada ya viungo kukolea unaweza kuwaoka kwenye ‘oven’ inayotumia umeme au ukatumia moto wa mkaa, pia unaweza kuwakaanga au kuwachemsha ukatengeneza supu tamu itakayosindikiza mihogo uliyoiandaa

Ukifika hapo utakuwa umemaliza mapishi ya futari ya mihogo na samaki kinachobaki ni kujipakulia na kufaidi utamu unaoweza kusindikizwa na uji au chai.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV