Jinsi ya kuishinda taharuki ya kirusi kipya cha Uviko-19
December 10, 2021 9:17 am ·
Mwandishi
Dar es Salaam. Kama wewe ni miongoni mwa watu ambao unahofia maisha yako kuhusu aina mpya ya kirusi cha Corona cha “Omicron” ambacho kimeripotiwa katika maeneo mbalimbali duniani. Fahamu kuwa mapambano dhidi ya kirusi hicho yanaendelea na hutakiwi kuwa na hofu, endelea na maisha yako kama kawaida.
Katika kipindi hiki, pata chanjo ya Uviko-19, vaa barakoa, nawa mikono na epuka mikusanyiko isiyo ya lazima.
