Jinsi mabadiliko ya tabianchi yanavyoigharimu Tanzania
- Takriban trilioni 1.2 zinahitajika kwa mwaka ili kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi.
Dar es Salaam. Tanzania ni moja ya nchi nyingi duniani zinazokumbana na athari za mabadiliko ya tabianchi ikiwemo kuongezeka kwa joto pamoja na kupungua kwa mvua.
Hali hiyo ambayo inaendelea kutishia maisha ya viumbe hai duniani, imesababisha kuongezeka kwa gharama za kitaifa hasa katika harakati za kukabiliana na athari zake.
Kwa mujibu wa Ripoti ya 3 ya Hali ya Mazingira Tanzania (2019) iliyotolea na Ofisi ya Makamu wa Rais, inaonesha kuwa mabadiliko ya tabianchi yanaigharimu Tanzania takriban asilimia 1 ya pato la Taifa, kiwango ambacho kinakadiriwa kitaongezeka hadi asilimia 2 ifikapo mwaka 2030.
Jambo la hatari zaidi ni kuwa joto linatarajiwa kuongezeka kati ya juzijoto 1 hadi 2 ifikapo 2030 na kusababisha ongezeko la magonjwa kikiwemo kipindupindu, hivyo kuweka rehani maisha wananchi, hatua zisipochukuliwa.

Latest
