Mabadiliko ya tabianchi yanavyohtarisha afya za binadamu duniani

March 16, 2022 10:31 am · Herimina
Share
Tweet
Copy Link
  • Takribani vifo 250,000 vitaongezeka kila mwaka ifikapo mwaka 2030-2050 kutokana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Dar es Salaam. Shirika la Afya Duniani (WHO) linaeleza kuwa  mabadiliko ya tabianchi ni moja ya tishio kubwa la afya ya binadamu kwa sasa.

Kwa mujibu wa Shirika hilo, kati ya mwaka 2030 na 2050, takribani vifo 250,000 vitaongezeka duniani kila mwaka kutokana na magonjwa yanayochochewa na mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo kipindupindu na Malaria.

Licha ya kuwa nchi zinazoendelea zinachangia kiasi kidogo katika mabadiliko ya tabianchi, WHO inaeleza kuwa nchi hizo ndizo zinaathirika zaidi na zitakuwa katika wakati mgumu wa kukabiliana na athari zake kutokana na mifumo duni ya huduma za kiafya.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW