Jifunze nguvu ya familia katika filamu ya “Coffee and Kareem”
- Ni filamu inayomhusu kijana mwenye miaka 12 anayetaka kutenganisha penzi la mama yake na mpenzi wake mpya.
- Safari yake inamfanya kuwa shuhuda wa mauaji na anaishia kuwa “panya kwenye nyumba ya paka”.
- Kiitikio cha filamu hii ni baada ya familia nzima kulazimika kukaa pamoja. Wataweza?
Dar es Salaam. Hata kabla ya jua kuchomoza, Kareem anamfuma mama yake na mpenzi wake wakiwa kwenye tendo la kuujaza ulimwengu. Ni tendo gani? Najua umeelewa!
Kijana huyo mwenye miaka 12 ambaye anaishi na mama yake pekee, hakufurahishwa na kitendo cha mama yake kuwa na mwanamume mwingine.
Hapo ndipo safari ya kuhakikisha uhusiano wa polisi James Coffee (Ed Helms) na mama yake Vanessa Manning (Taraji Henson) unafikia ukingoni.
Kareem anatafuta kundi maalum la kumpatia Coffee kipigo cha mbwa koko ili aachane na mama yake. Akiwa katika safari hiyo, anaona yasiyopaswa kuonekana.
Lahaula! Kitumbua kimeingia mchanga kwani Kareem ameshuhudia mauaji na ni shahidi anayetafutwa na kundi la nguli wa kuuza madawa ya kulevya kwenye mji wa Detroit nchini Marekani.
Sio yeye tu, ni Kareem na Coffee wanaotafutwa na genge la wahalifu wakiwemo Rodney (King Bach) na Orlando Johnson (RonReaco Lee).
Zinazohusiana
- Hapa ndipo uhalifu unapowaunganisha wapendanao
- Unatafuta filamu ya wikiendi? Confidential Spenser inakusubiri
- Filamu ya “The Love Birds” inakusubiria kuipamba wikiendi yako
Hali inazidi kuwa mbaya baada ya mama kuingia kwenye mchezo huo wa paka na panya unaolazimu watatu hao kukaa pamoja.
Unahitaji kuvunja mbavu wikiendi hii, mwachie hiyo kazi Kareem na wazazi wake kwenye filamu ya “Kareem and Cofee” inayopatikana katika mtandao wa Netflix.
Umelipia kifurushi chako? Usisahau kukitumia kwa kutazama filamu hii ya muda wa saa 1:28.
Latest