Je unakumbuka njia za kujikinga na Uviko-19?
- Nenda kapate chanjo ya ugonjwa huo.
- Nawa mikono, vaa barakoa na epuka mikusanyiko ya watu wengi.
Dar es salaam. Ni takribani miaka mitatu sasa tangu ugonjwa wa Corona (Uviko-19) uikumbe dunia na kusababisha watu kuugua na wengine hata kufa.
Katika mahojiano na waandishi wa habari jijini Geneva Uswisi, Agosti 25 mwaka huu, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dk. Tedros Ghebreyesus alitoa wito kwamba watu hawapaswi kujisahau wala kuchukulia kama janga la Uviko-19 limeisha kwa sababu linaendelea kuua mamilioni ya watu duniani.
Hata hivyo serikalii duniani zimeendelea na juhudi mbalimbali za kupambana na janga hilo ikiwemo utoaji chanjo kwa watu wa rika mbalimbali.
Jitihada hizi za kukabiliana na Uviko-19 hazipaswi kufanywa na serikali tu lakini watu pia kushirikishwa kukabiliana na janga hili la ulimwengu.
Soma zaidi
Mambo muhimu ya kuzingatia kujikinga na Corona
1. Kumbuka kunawa mikono kila mara kwa kutumia sabuni na maji tiririka kwa angalau sekunde 20, ama tumia kitakasa mikono. Kwa kufanya hivyo utakuwa unajikinga na Uviko-19.
2. Kumbuka kuvaa barakoa unapokua sehemu zenye watu wengi kama vile sokoni ama kwenye usafiri wa umma. Hii ni muhimu hasa katika maeneo yenye maambukizi makubwa ya ugonjwa huo.
3. Epuka kushika macho, pua, ama mdomo wako. Hii itasaidia kupunguza uwezekano wa kusambaza virusi kwenye maeneo hayo ambayo ndio njia kuu ya kupitisha virusi hivyo.
4. Funika mdomo wako na pua kwa kutumia kiwiko ama tishu unapokohoa ama kupiga chafya. Tupa tishu sehemu salama baada ya kuitumia.
5. Kumbuka kukaa umbali kati yako na watu wengine kadiri inavyowezekana. Hii inamaanisha kukaa umbali wa mita 2 kati yako na watu wengine, haswa wale wenye dalili za kuumwa.
Latest
