Guterres: Hakuna jamii itakayokuwa huru na haki bila waandishi wa habari

October 9, 2021 7:02 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Vyombo vya habari ndiyo msingi wa demokrasia ya kweli.
  • Ataka vyombo vya habari viheshimiwe na kulindwa.
  • Wapongeza wanahabari wawili waliopata tuzo ya Nobel mwaka 2021.

Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Antonio Guterres amewapongeza waandishi wa habari Maria Ressa na Demirty Muratov kwa kushinda tuzo ya amani ya Nobel mwaka huu akisema uhuru wa vyombo vya habari ni muhimu katika ujenzi wa demokrasia duniani.

Maria, mwandishi wa habari za uchunguzi wa Ufilipino na mwandishi wa habari wa Urusi, Muratov wametunukiwa tuzo ya Nobel kwa mwaka 2021 kwa kuwa mstari wa mbele kulinda uhuru wa kujieleza duniani licha ya changamoto wanazokutanazo katika shughuli zao.

“Duniani kote uhuru wa vyombo vya habari ni muhimu kwa ajili ya amani, haki, maendeleo endelevu na haki za binadamu na ni ngumo muhimu kwa ajili ya ujenzi wa taasisi zenye haki na zisizo na upendeleo,” amesema Guterres. 

Katika taarifa yake ya Oktoba 8, 2021 ya pongezi kwa washindi hao, Guterres amesisitiza kuwa “hakuna jamii inayoweza kuwa huru na haki bila waandishi wa habari ambao wanaweza kuchunguza maovu, kufikisha taarifa kwa umma, kuwawajibisha viongozi na kuzungumza ukweli kwa mamlaka.” 

Licha ya ukweli huo bado vyombo vya habari vinaendelea kupingwa na mashambulizi dhidi ya wanahabari yanaendelea kuongezeka duniani. 

“Tunashuhudia machafuko yakiongezeka na unyanyasaji dhidi ya waandishi wa habari wa ana kwa ana au mtandaoni. Wanawake waandishi wa habari mara nyingi ndiyo walengwa wa ukatili huo,” amesema. 

Katibu Mkuu amesema wakati huo huo teknolojia imebadili njia za watu kupokea na kubadilishana taarifa , pia inatumika kupotosha maoni ya umma au kuchochea machafuko na chuki. 

“Uongo  wa kupinga ukweli, na hii haiwezi kuwa kawaida mpya. Uandishi wa habari huru na wa kujitegemea ni mshirika wetu mkubwa katika kupambana na habari potofu na upotoshaji,” amesisitiza Guterres.

Amezitaka serikali duniani kutambua jukumu la msingi la waandishi wa habari na kuelimarisha juhudi katika kila ngazi kusaidia vyombo vya habari huru vya kujitegemea na vya aina mbalimbali. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Nukta TV

Sakata bei ya mafuta kupanda latua BoT, Naibu Gavana atoa ufafanuzi

Sakata bei ya mafuta kupanda latua BoT, Naibu Gavana atoa ufafanuzi

Nukta TV

BoT yabakiza Riba ya Benki Kuu 5.75% kudhibiti mfumuko wa bei

BoT yabakiza Riba ya Benki Kuu 5.75% kudhibiti mfumuko wa bei

Nukta TV