Ghana yawa nchi ya kwanza kupokea chanjo ya COVID-19 chini ya programu ya Covax

February 25, 2021 6:46 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Shehena ya kwanza ya chanjo aina ya AstraZeneca / Oxford zilizotolewa COVAX imewasili nchini humo jana Februari 24, 2020.
  • Programu hiyo maalum ya COVAX inayosimamiwa na Umoja wa Mataifa (UN) inakusudia kuhakikisha chanjo zinapatikana kwa kila mtu na kwa gharama nafuu.

Ghana imekuwa nchi ya kwanza duniani na barani Afrika kupokea chanjo dhidi ya virusi vya Corona chini ya programu maalum ya COVAX inayosimamiwa na Umoja wa Mataifa (UN) inakusudia kuhakikisha chanjo zinapatikana kwa kila mtu na kwa gharama nafuu.

Hatua hiyo inakuja baada ya Waghana zaidi ya 80,700 kuambukizwa ugonjwa huo na zaidi ya 580 kufariki dunia, hatimaye mwelekeo wa kuondokana na janga hilo umeanza kuonekana nchini humo. 

Shehena ya kwanza ya chanjo aina ya AstraZeneca / Oxford zilizotolewa na COVAX imewasili nchini humo jana Februari 24, 2020.

“Chanjo hizo 600,000 ni sehemu ya mpango wa awali ya kusambaza chanjo kupitia mfumo wa COVAX na zimetokana na leseni kwa taasisi ya Serum ya India na inawakilisha awamu ya kwanza ya chanjo za COVID-19 zinazoelekezwa nchi za kipato cha chini na kati,” amesema mwakilishi wa shirika la kuhudumia watoto (UNICEF) nchini Ghana, Dk Francis Kasolo baada ya shehena hiyo kuwasili. 


Zinazohusiana:


Akihojiwa na redio ya Umoja wa Mataifa, Dk Kasolo amesema kuwa njia pekee ya kuondokana na janga hili ni kuhakikisha chanjo zinapatikana kwa kila mtu popote aliko.

Kuwasili kwa shehena hiyo pia ni mwanzo wa operesheni kubwa zaidi ya kusambaza chanjo duniani ili kuokoa maisha ya watu na uchumi wa dunia.

Mfumo wa COVAX unapanga kusambaza takribani chanjo bilioni 2 za chanjo dhidi ya COVID-19 mwaka huu pekee huku malengo ni kumfikia kila mkazi wa dunia.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV