Fanya haya kuepuka msukumo wa makundi rika wakati wa Uviko-19
- Ni pamoja na kujiepusha na makundi sogozi yanayotuma habari za uzushi.
Dar es Salaam. Katika kipindi cha mlipuko wa ugonjwa wa Corona (Uviko-19), kila mtu ana jambo ambalo amelishikilia kama imani yake. Baadhi wameamua kupuuzia tahadhari ya ugonjwa huo huku wengine wakisita kupata chanjo.
Hayo hutokea kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kukosa taarifa sahihi, msukumo hasi wa kundi fulani la watu na wakati mwingine ni matokeo ya habari za uzushi kuhusu ugonjwa huo.
Vijana huiita hali hiyo “kujazana ujinga”.
Wakati inaweza kuwa jambo zuri kuwasikiliza washikaji zako, huenda ukawa unashindwa kusikiliza kitu kikubwa zaidi, nafsi yako.
Ni muhimu kufahamu kuwa rafiki yako asipopata chanjo na asipate maambukizi ya Uviko-19 haimaanishi kuwa na wewe utakuwa na bahati hiyo.
Hayo yote ni kwa sababu wewe na rafiki yako mnatofautiana mazingira, kipato, shughuli za kufanya mara baada ya kila mtu kurudi kwao.
Ili kuepuka msukumo wa makundi rika , inashauriwa kuwasikiliza zaidi wataalamu hasa linapokuja kwenye masuala ya afya yako.
Latest