Tamisemi yaomba Sh9.14 trilioni

April 14, 2023 8:39 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Fedha hizo ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo mwaka 2023/24. 
  • Asilimia 38.1 ya bajeti hiyo kuelekezwa katika miradi ya maendeleo. 

Dar es Salaam. Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imeliomba Bunge liidhinishe Sh9.1 trilioni kwa matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo kwa mwaka 2023/24 ikiwa ni ongezeko la Sh366 bilioni kutoka bajeti iliyoombwa ya mwaka jana. 

Waziri wa Tamisemi Angellah Kairuki aliyekuwa akisoma hotuba ya makadirio na mapato ya wizara hiyo kwa mwaka 2023/24  leo Aprili 14, 2023 amewaambia wabunge kuwa kati ya fedha hizo Sh5.6  ni kwa ajili ya shughuli za kawaida huku Sh3.48 trilioni ni kwa ajili matumizi ya maendeleo.

Sasa naomba Bunge lako Tukufu likubali kuidhinisha Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2023/24 jumla ya Sh9.144 trilioni kati ya fedha hizo Sh5.65 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida yanayojumuisha mishahara ya walimu.

“Sh3.48 trilioni kwa ajili ya shughuli za maendeleo na Sh 1.06 kwa trilioni kwa ajili ya matumizi mengineyo,” amesema Kairuki bungeni jijini Dodoma.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.