Fahamu mishahara mipya ya wafanyakazi wa ndani, hotelini

December 6, 2022 2:51 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Dar Dar es Salaam. Serikali imetangaza viwango vipya vya kima cha chini cha mishahara kwa wafanyakazi wa ndani na hotelini ambavyo vitaanza kutumika Januari 1, 2023.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,  Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako katika tangazo lilitolewa katika Gazeti la Serikali, amesema viwango hivyo ni kwa sekta binafsi. 

Viwango hivyo vitawanufaisha zaidi wafanyakazi wa kazi za ndani wale wasioajiriwa na wanadiplomasia, wafanyabiashara wakubwa na maafisa wenye stahiki ambapo watakuwa wanalipwa Sh60,000 kwa mwezi kuanzia mwaka ujao. 

Kiwango hicho kimeongezeka kutoka Sh40,000 waliyokuwa wakilipwa hapo awali kwa mujibu wa Takwimu muhimu za Tanzania za mwaka 2018 zilizotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).

Wafanyakazi wa ndani wanaoilipwa kima cha chini cha mshahara cha juu kuliko wengine ni wale wafanyakazi wa kazi za ndani walioajiriwa na wanadiplomasia na wafanya biashara wakubwa. Kwa mujibu wa tangazo hilo watalipwa Sh250,000. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Nukta TV

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

Nukta TV

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Nukta TV