Fahamu ‘kisima’ cha taarifa za chanjo za corona duniani

June 16, 2021 1:14 pm · Daniel
Share
Tweet
Copy Link
  • Unaweza kujua ni chanjo ngapi zimetengezwa na ngapi zimeruhusiwa.
  • Kupitia mfumo huu utaweza kujua kila hatua ya chanjo iliyokuwa katika majaribio.

Dar es Salaam.Tangu chanjo ya ugonjwa wa virusi vya corona (Covid-19) ipatikane kumekuwa na sintofahamu kubwa inayosababisha kusambaa kwa taarifa nyingi za uzushi dhidi ya chanjo hiyo muhimu katika maisha ya binadamu. Hali hiyo imefanya  mashirika, kampuni na taasisi mbalimbali ulimwenguni kuja na mikakati ya kukabiliana na habari hizo.

Miongoni mwa mashirika hayo ni Shirika la Habari la Marekani la New York Times liliounda mfumo wa kidigitali  ujulikanao kama “Coronavirus Vaccine Tracker” ukiwa ni mfumo wenye taarifa lukuki kuhusu chanjo za corona.

Mfumo huo unaeleza mambo mbalimbali ikiwemo idadi ya chanjo zilizotengezwa na zile zilizofanyiwa majaribio.

Pia mfumo huo wa unaeleza ni chanjo gani zimeruhusiwa kutumiwa na zimetengenezwa na kutoka nchi gani na taasisi gani huku zikiwa na maelezo ya ziada ya kitabibu kuhusu utumiaji wake.

Miongoni mwa taarifa hizo ni idadi ya mtu kufikia kiwango kamili cha chanjo inayotakiwa kumkinga kikamilifu dhidi ya maradhi hayo yanayozidi kuutesa ulimwengu.

‘Coronavirus Vaccine Tracker’ ni moja ya mifumo mizuri inayosaidia kutoa elimu ya chanjo kwa kiasi kikubwa ulimwenguni hivyo pale unapokutana na taarifa unayoitilia mashaka huna budi kutembelea katika mfumo huu na kuweza kujiridhisha uhakika wa taarifa hizo .

Hadi sasa Shirika la Afya Duniani (WHO) limeruhusu chanjo za Astra Zeneca/Oxford vaccine, Johnson and Johnson, Moderna,  Pfizer/BionTech, Sinopharm na  Sinovac kutumika ulimwenguni ili kuwakinga watu na maradhi ya Covid-19.

Miongoni mwa chanjo hizi zinatumiwa na baadhi ya mataifa ya jumuiya ya Afrika Mashariki kama Kenya, Uganda na Rwanda ambazo zimeanza kuwachanja raia wake.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV