Dk Mabula: Wasakwe kokote walipo warudi shuleni

February 20, 2023 11:47 am · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link

Mbunge wa Jimbo la Ilemela Dk Angeline Mabula akikagua ujenzi wa bweni la wasichana katika Shule ya Sekondari Igogwe. Mbunge huyo yupo jimboni kwake akikagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Picha | Mariam John.


  • Ni wanafunzi saba ambao hawajaripoti kidato cha kwanza Shule ya Sekondari Igogwe.
  • Waziri wa Ardhi aagizwa wasakwe wao na wazazi wao.

Mwanza. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Angeline Mabula amewaagiza watendaji kuhakikisha wanawatafuta wanafunzi saba ambao bado hawajaripoti kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Igogwe wilayani Ilemela mkoani Mwanza.

Waziri Mabula ametoa agizo hilo alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya kupunguza umasikini (TPRPIV- OPEC) jimboni kwake na kueleza kuwa zipo taarifa za baadhi ya wanafunzi hao kutoroka nyumbani na wengine kuolewa.

“Hao watoto saba na wazazi wao lazima wapatikane kama kushitakiwa anashitakiwa mzazi na mtoto, haiwezekani Rais anatoa fedha ya kutosha ya kuweka miundombinu Sh516 milioni kwa Kata moja, lakini wao hawaripoti shule,” ameeleza Dk Mabula.

Ameeleza kuwa katika shule hiyo, ilipangiwa wanafunzi 167 wa kidato cha kwanza kwa mwaka wa masomo wa 2023, kati yao 160 wameripoti shuleni na waliobaki hawajaripoti na sababu zikielezwa kuwa baadhi yao wameolewa na wengine walitoroka nyumbani.

Amesema suala la shule sio la kuchukulia mzaha hasa kipindi hiki ambapo Serikali inaboresha miundombinu ya shule. 

Pia ameeleza kuwa wanataka watoto wote waendelee na masomo hawataki kuona mtoto anaishia darasa la saba.

“Kwenye elimu hatutaki mchezo tunachohitaji watoto wote wasome, niwapongeze kuwa ni kiwago kidogo cha wanafunzi ambao hawajaripoti lakini taarifa zao siyo nzuri kwa sababu wengine wameolewa, wengine wamekimbia hapana lazima wapatikane na bahati nzuri Rais aliisha ridhia  mtoto akipata ujauzito anapata fursa ya kuendelea na masomo watafutwe waendelee na shule,” ameeleza waziri huyo.

Awali Mkuu wa shule ya sekondari Igogwe Atanas Manyika amesema shule hiyo kwa mwaka mpya wa masomo 2023 ilipangiwa wanafunzi 167.

“Hatuna taarifa rasmi sana lakini zilizopo zinasemekana kuwa wengine wameolewa na wengine walitoroka baada ya kumaliza darasa la saba ,tayari tumeanza kuchukua hatua ikiwemo kupeleka taarifa zao ngazi za juu,” amesema Manyika

Mbali na ziara hiyo pia Waziri huyo amekagua ujenzi wa barabara ya Kahama kuelekea Shibula, barabara ya Igombe mwaloni, zahanati ya Mihama pamoja na eneo la ujenzi wa zahanati mpya katika kata ya Kitangiri.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV