CAG Kichere alivyojipanga kuendeleza kazi ya Prof Assad

November 5, 2019 11:00 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Amesema kuwa ataendelea kutekeleza majukumu ambayo yameachwa na CAG aliyemaliza muda wake, Prof Mussa Assad.
  • Amesema atahakikisha kuwa analinda kodi ya Watanzania ili iweze kunufaisha makundi yote.

Dar es Salaam. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) mpya, Charles Kichere amesema kuwa ataendelea kutekeleza majukumu ambayo yameachwa na CAG aliyemaliza muda wake, Prof Mussa Assad kwani Ofisi hiyo ni muhimu kwa maendeleo ya Watanzania.

Akizungumza katika makabidhiano ya ofisi leo (Novemba 5, 2019) jijini Dar es Salaam, Kichere amesema kuwa Ofisi ya CAG ni nguzo muhimu kwa Watanzania kwani ndiyo ofisi inayolinda na kuangalia matumizi sahihi ya kodi yao wanayolipa kila siku.

“Niwaahidi kwanza tutaendelea kufanya kazi hii ambayo ambayo imefanywa na Prof Assad na timu yake, nitahakikisha kushirikiana na wafanyakazi wa Ofisi hii kwa umakini mkubwa sana.

Tutafanya kazi hii kwa kuzingatia weledi, uadilifu kama alivyosema Profesa. CAG huwa siye anayefanya kazi, CAG anawajibika kwa kusaini ripoti, lakini ripoti inaanzia chini kwa wafanyakazi,” amesema CAG Kichere.  

Kichere amesema kuwa katika kutekeleza majukumu hayo mapya atahakikisha kuwa atalinda kodi ya Watanzania ili iweze kunufaisha makundi yote ikiwemo wakulima, wafugaji, wavuvi, wafanyabiashara na wafanyakazi. 

“Nataka kufanya kazi kulinda maslahi ya Watanzania, nimefanya kazi Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) najua ugumu wa kukusanya kodi na kupata mapato, kwa hiyo nitahakikisha kuwa nailinda kodi ya wananchi kwa wivu mkubwa sana”, amesisitiza Kichere.


Zinazohusiana:   


Kichere aliteuliwa kuwa CAG Novemba 3 akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Profesa Mussa Assad ambaye anamaliza muda wake wa miaka mitano.

Kabla ya Kichere kuteuliwa kuwa CAG alikuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe na kabla ya hapo alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na nafasi yake ilichukuliwa na  Edwin Mhede. 

CAG aliyemaliza muda wake Prof Mussa Assad amesema kuwa ataendelea kushirikiana na Ofisi hiyo licha ya kustaafu lakini atakuwepo kwa wakati ambao atahitajika kutoa msaada kutokana na uzoefu na ujuzi aliopata kwa muda wa miaka mitano akiwa anatumikia ofisi hiyo.

“Nataka nikuambie CAG mpya ukihitaji msaada wa kitu chochote kiwe cha binafsi au cha kiofisi, ujuzi na uzoefu wa kazi hii niko tayari kushirikiana na wewe na utapata msaada huo kwa haraka”, Alisema Prof. Assad.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Nukta TV

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Nukta TV

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV