Biashara ya hewa ukaa inavyoweza kuokoa mazingira Tanzania

May 29, 2021 10:22 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Inahusisha udhibiti wa uzalishaji wa gesi joto duniani.
  • Gesi hizo huchangia kuongeza joto la dunia na hewa ukaa.
  • Biashara hiyo inahusisha upandaji wa miti na kudhibiti shughuli za uzalishaji hewa ukaa.

Morogoro. Wataalam wa mazingira wameshauri watu binafsi, taasisi, mashirika na kampuni binafsi nchini Tanzania kufanya biashara ya hewa ukaa (carbon trading) ili kupunguza uchafuzi wa hewa na ongezeko la joto duniani jambo litakalosaidia kutunza mazingira.

Biashara ya hewa ukaa ni mfumo katika soko la dunia ambao unakusudia kupunguza gesi joto ambazo zinachangia kuongezeka kwa joto la dunia hasa ikiwemo hewa ukaa (carbondioxide) ambayo inatokana na shughuli za viwanda na uchomaji wa uoto na ukataji wa miti.

Mkurugenzi wa Kituo cha Kitaifa cha Kufuatilia Kaboni (NCMC) Prof Eliakimu Zahabu amesema kwa sasa dunia ikiwemo Tanzania inakabiliwa na athari nyingi za mabadiliko ya tabianchi ambayo yamesababishwa na kuongezeka kwa viwango vya hewa ukaa. 

Athari hizo ni pamoja na ongezeko la joto la dunia, ukame, mafuriko, ukosefu wa malisho kwa wafugaji na kuteteleka kwa shughuli za kilimo na uvuvi ambazo ni vyanzo vya mapato kwa wakulima. 

Prof Zahabu amesema njia mojawapo ya kukabiliana na ongezeko la hewa ukaa ni kuanzisha miradi ya biashara ya hewa hiyo katika maeneo mbalimbali Tanzania. Biashara hiyo inahusisha upandaji na utunzaji wa miti na kuweka mifumo inayodhibiti uzalishaji wa hewa ukaa katika shughuli mbalimbali katika sekta za kilimo, nishati, viwanda, miundombinu.

“Biashara ya hewa ukaa inasisitizwa duniani na Umoja wa Mataifa kwa sababu kiwango cha hewa ukaa kimeongezeka sana na kinatishia maisha ya binadamu na viumbe wengine wanaotegemea mazingira kuishi,” alisema Prof Zahabu katika warsha ya wanahabari kuhusu hewa ukaa iliyofanyika Mei 28, 2021 mkoani Morogoro.


Zinazohusiana: 


Baadhi ya miradi inayoanza kufanya biashara hiyo Tanzania ni pamoja na mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam (DART) na Carbon Tanzania uliopo mkoani Arusha ambao unawahamasisha wananchi kutunza na kupanda miti katika maeneo yao ili kufyoza hewa akaa isisambae angani.

Hata hivyo, Prof Zahabu ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) amesema biashara hiyo ili ifanikiwe inahitaji kutimiza vigezo vya kimataifa na kupata kibali cha nchi husika. 

“Miradi hii inahitaji rasilimali za kutosha zikiwemo fedha na kufanya utafiti wa kina ili ukidhi viwango vya kimataifa vinavyosimamia biashara hiyo,” amesema mtaalam huyo wa mazingira.

Biashara hiyo inasimamiwa na Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Mkataba wa Kudhibiti Mabadiliko ya Hali ya Hewa (UNFCCC), ambapo kigezo kimojawapo kinachohitajika ni kuandika andiko litakalohusisha makundi yote yaliyopo katika mradi na kisha wahusika wakubaliwe na nchi husika kufanya mradi huo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
6 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
6 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV