Bei ya mahindi yapaa Morogoro

January 17, 2022 2:02 pm · Wilson
Share
Tweet
Copy Link
  • Bei ya mahindi yapaa kwa asilimia 56 Mkoa wa Morogoro
  • Tabasamu zaidi kwa wakulima na wafanya biashara na vilio kwa walaji.

Dar es salaam. Bei ya jumla ya mahindi katika mkoa wa Morogoro imepada katika kipindi cha wiki moja,  jambo linalowapa kicheko wakulima na wafanyabiashara.

Takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa leo (Januari 14, 2022) na Wizara ya Viwanda na Biashara zinaonyesha kuwa bei ya juu ya gunia la kilo 100 la zao hilo mkoani humo linauzwa kwa Sh150,000 kutoka Sh66,604 kama ilivyorekodiwa wiki iliyopita Januari 10, 2022. 

Hilo ni sawa na ongezeko la asilimia 56 (Sh66,604) ndani ya kipindi cha wiki moja.

Kupanda kwa bei ya zao hilo katika Mkoa wa Morogoro huenda kukabadili mwelekeo wa kibiashara katika masoko mbalimbali hususani yaliyo jirani na Mkoa huo na kuwaingizia faida zaidi wakulima na wafanyabiashara.

Bei inayotumika leo mkoani Morogoro ndiyo ya juu zaidi Tanzania Bara huku bei ya chini ikirekodiwa mkoani Ruvuma kwa Sh50,000. 


Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW