Ahueni, Serikali ikitangaza kuongeza vituo 10 vya CNG Dar, Mtwara, Moro
- Wachambuzi wapongeza hatua hiyo, wasema watumiaji wa usafiri binafsi ndio wtakaonuaika zaidi.
Arusha. Huenda wamiliki wa vyombo vya moto nchini Tanzania vinavyotumia gesi asilia iliyoshinikizwa (CNG) wakapata ahueni kiduchu mara baada ya Serikali kutangaza mpango wa kuongeza vituo10 vya gesi hiyo nchini.
Mpango huo unaotarajiwa kutekelezwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), kwa kushirikiana na sekta binafsi umebainishwa na Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba katika kipindi cha maswali na majibu bungeni Dodoma jana Mei 28, 2026.
Salome amebainisha kuwa vituo hivyo vitajengwa katika mikoa mitatu ambapo ya Dar es Salaam, Mtwara na Morogoro pamoja na kukamilisha taratibu za ununuzi wa vituo vitano vya gesi visivyohamishika katika mikoa mingine mitatu.
Ikiwa mpango huo utakamilika Tanzania itakuwa na jumla ya vituo 28 vy CNG vitakavyorahisisha utoaji wa huduma hiyo kutoka vituo 18 vilivyopo sasa.