Dola ya Marekani yaimarika kwa Sh5 NMB, CRDB yabaki tulivu
- Hii inamaanisha kuwa wanunuaji wa dola kupitia benki ya NMB watalazilima kutoboa mfuko zaidi kulinganisha na jana.
Dar es Salaam. Dola ya Marekani (USD) imeimarika kwa Sh5 katika Benki ya NMB, huku ikiendelea kudumisha viwango vyake bila mabadiliko katika benki ya CRDB.
Kwa mujibu wa takwimu za viwango vya ubadilishaji fedha vinaonesha leo Julai 29, 2026 Dola ya Marekani imenunuliwa kwa Sh2,600 na kuuzwa kwa Sh2,680 katika benki ya CRDB, viwango sawa na jana.
Kwa upande wa Benki ya NMB, Dola ya Marekani imeonesha ongezeko la Sh5 huku kiwango cha bei ya kununua kikifika Sh2,605 na Sh2,685 kwa bei ya kuuza.
Hii inamaanisha kuwa wanunuaji wa dola kupitia benki ya NMB watalazilima kutoboa mfuko zaidi kulinganisha na jana.
Hata hivyo, kwa wateja watakao uza dola kupitia benki hiyo ongezeko hilo ni manufaa kutunisha mifuko kwa kupata kiasi kikubwa zaidi cha Shilingi ya Tanzania.
