Dola ya Marekani tulivu kwa miezi mitatu Tanzania
- Ilikuwa ikishuka kwa wastani wa Sh25 ka bei ya kuuza na Sh5 kwa bei ya kununua.
Dola ya Marekani imeendelea kuwa tulivu dhidi ya shilingi ya Tanzania ndani ya miezi mitatu mfululizo kuanzia Mei 3, 2026.
Uchambuzi uliofanywa na Nukta Habari umebaini kuwa ndani yta kipindi hicho Dola ya Marekani ilikuwa ikishuka kwa wastani wa Sh25 ka bei ya kuuza na Sh5 kwa bei ya kununua.
Mei 3, 2026 Fedha hiyo yenye nguvu duniani iliuzwa kwa kupitia 2,650 na kununuliwa kwa Sh2,570 kupitia Benki ya CRDB.
Leo Julai 13, 2026 Kupitia Benki ya CRDB na NMB Dola moja ya Marekani imeuzwa kwa Sh2,675 na kununuliwa kwa Sh2,595.
Mwenendo huo tulivu unaweza kupunguza maumivu kwa Watanzania wanaoagiza mizigo na bidhaa kutoka nje, hali itakayofanya iwe rahisi zaidi kwa wanunuaji wa reja reja wa bidhaa hizo nchini.
