Dola ya Marekani tulivu,sarafu nyingine zaongezeka kidogo Juni 10, 2026
- Sarafu nyingine zilizoonyesha mabadiliko kidogo ni pamoja na GBP , CNY na INR.
Dar es Salaam. Dola ya Marekani imeendelea kuwa tulivu katika soko la fedha za kigeni nchini, ndani ya wiki mbili zilizopita kuanzia Mei 30, 2026.
Katika viwango vinavyotumika leo Juni 10, 2026, fedha hiyo inayoshika hatamu duniani imenunuliwa kwa Sh2,585 na kuuzwa kwa Sh2,665 kupitia Benki ya CRDB, huku Benki ya NMB ikinunua kwa Sh2,580 na kuuza kwa Sh2,660, viwango ambavyo vimebaki imara bila mabadiliko tangu jana.
Wakati Dola ikiendelea kutulia, baadhi ya sarafu za kimataifa zimeonyesha ongezeko dogo la thamani dhidi ya Shilingi ya Tanzania.
Sarafu ya Umoja wa Ulaya (Euro) katika Benki ya CRDB imenunuliwa kwa Sh2,875.91 na kuuzwa kwa Sh3,175.91 kutoka Sh2,866.81 iliyokuwa ikinunuliwa na kuuzwa ya Sh3,166.81 iliyotumika jana.
Sarafu nyingine zilizoonyesha mabadiliko kidogo ni pamoja na Pauni ya Uingereza (GBP) Yuan ya China (CNY) na Rupia ya India (INR).
Mabadiliko hayo yanaonyesha kuwa licha ya utulivu wa Dola ya Marekani, baadhi ya sarafu za kimataifa zimeendelea kupata nguvu kidogo dhidi ya Shilingi ya Tanzania katika biashara ya leo ya fedha za kigeni.
