Soko la fedha za kigeni laendelea kuonyesha utulivu Tanzania

April 27, 2026 11:51 am · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Viwango vya kubadilisha fedha za kigeni dhidi ya Shilingi ya Tanzania vimeendelea kuonyesha utulivu katika wiki ya mwisho ya Aprili, huku baadhi ya sarafu zikibaki katika viwango vilevile vilivyorekodiwa wiki iliyopita.

Kwa mujibu wa viwango vya kubadilisha fedha za kigeni vilivyotolewa na Benki za NMB na CRDB leo Aprili 27,2026  Dola ya Marekani (USD) imeendelea kununuliwa kwa Sh2,570 na kuuzwa kwa Sh2,650 ikiwa ni sawa na kiwango kilichorekodiwa wiki iliyopita.

Hata hivyo, uchambuzi wa mwenendo wa viwango hivyo ndani mwezi mmoja kuanzia Machi 27 unaonesha kuimarika kwa Dola ya Marekani kutoka Sh2,635 iliyotumika kuuza sarafu hiyo na kununuliwa kwa Sh2,555 katika benki zote mbili.

Sarafu nyingine ikiwemo Euro zimeonesha mabadiliko kidogo ikishuka katika Benki ya CRDB kutoka Sh2,931.77 (kununua) hadi Sh2,899.8, na kutoka Sh3,231.77 (kuuza) hadi Sh3,199.8 kulinganisha jumatatu iliyopita Aprili 20, 2026. 

Hali kama hiyo imeonekana pia kwa Rand ya Afrika Kusini (ZAR) na Rupia ya India (INR) ambazo zimepungua kwa viwango vidogo.

Kwa upande mwingine, baadhi ya sarafu katika Benki ya NMB zimeendelea kubaki karibu na viwango vya awali, zikionyesha mabadiliko yasiyo makubwa yenye kuashiria soko lenye utulivu.

Utulivu huu wa viwango unaashiria uwiano kati ya mahitaji na upatikanaji wa fedha za kigeni nchini, hali inayoweza kusaidia kudhibiti mfumuko wa bei, hasa kwa bidhaa zinazoagizwa kutoka nje.

Kwa wafanyabiashara wanaoagiza bidhaa nje ya nchi, kutokuwepo kwa mabadiliko makubwa kunarahisisha upangaji wa gharama na kupunguza hatari ya kupanda kwa bei ghafla. Aidha, wawekezaji hupata mazingira yenye uhakika zaidi wa kufanya maamuzi ya kifedha.

Kwa upande wa Serikali, mwenendo huu unaweza kuashiria uimara wa sera za fedha na usimamizi mzuri wa akiba ya fedha za kigeni, ingawa hali hii inaweza kubadilika kulingana na mwenendo wa soko la dunia, hususan thamani ya dola ya Marekani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

/
No matches found for this filter
22 May, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
23 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
23 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MIKOA YA KIPOLISI ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI TANZANIA BARA 2025

MIKOA YA KIPOLISI ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI TANZANIA BARA 2025

Nukta TV

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

Nukta TV

MIKOA 5 ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI 2025 TANZANIA BARA

MIKOA 5 ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI 2025 TANZANIA BARA

Nukta TV