Rais Samia ateua wanne kuwa wenyeviti wa bodi

February 11, 2026 5:42 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Walioteuliwa ni pamoja na Makinda, Dk Chuwa, Machano na Prof Maboko.

Arusha. Rais Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa vigogo wanne kuwa wenyeviti wa bodi mbalimbali kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dk Moses Kusiluka.

Taarifa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu iliyotolewa leo Februari 11, 2026 inabainisha kuwa Anne Samamba Makinda ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).

Makinda aliyewahi kuwa kushika nyadhifa kubwa nchini Tanzania ikiwemo Spika wa Bunge kuanzia mwaka 2010 hadi mwaka 2015 ameteuliwa katika nafasi hiyo baada ya kuhudumu katika nafasi ya kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022.

Wengine ni Jaffer Machano aliyeteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC) akichukua nafasi ya Ally Amani Karavina.

Aidha, Rais Samia pia amemteua Dk Albina Andrew Chuwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha Taifa cha Ufuatiliaji wa Kaboni (NCMC) na Prof Makenya Abraham Maboko kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU).

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.