TRA kuzindua mfumo mpya wa kodi utakaotumia AI 

January 5, 2026 6:32 pm · Goodluck Gustaph
Share
Tweet
Copy Link
  • Mfumo huo unatarajiwa kuongeza ufanisi, uwazi na kupunguza mianya ya upotevu wa mapato ya Serikali.

Dar es Salaam: Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inatarajia kuzindua mfumo mpya wa kodi unaotumia teknolojia ya akili bandia (AI) ujulikanao kama Integrated Domestic Revenue Administration System (IDRAS), kwa lengo la kuboresha usimamizi wa kodi na kurahisisha huduma kwa walipakodi.

Hayo yamebainishwa leo Januari 5, 2026 na Kamishina Mkuu wa TRA Yusuph Mwenda katika mkutano wa tathmini ya utendaji kazi wa TRA kwa nusu ya mwaka wa fedha 2025/2026, uliofanyika jijini Arusha.

Akizungumza katika mkutano huo, Kamishna Mwenda amesema mfumo huo mpya utafanyika kwa njia ya mtandao hivyo utapunguza ulazima wa walipakodi kufika ofisini mara kwa mara.

“Mfumo wa IDRAS utaondoa changamoto ya wafanyabiashara kukutana mara kwa mara na maafisa wa TRA, kwani huduma nyingi zitapatikana mtandaoni, lengo ni kuwapa wafanyabiashara muda zaidi wa kuendesha shughuli zao badala ya kuja ofisini kwetu,” amesema Kamishna Mwenda.

Aidha, amebainisha kuwa mfumo huo utatumia teknolojia ya akili bandia(AI) kufanya uchambuzi wa taarifa za kodi, hatua itakayosaidia kuongeza ufanisi, uwazi na kupunguza mianya ya upotevu wa mapato ya Serikali.

Kwa upande wake, Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar aliyekuwa mgeni rasmi katika mkutano huo ameitaka TRA kuendelea kuimarisha mifumo yake ya Tehama kwa kujilinganisha na nchi nyingine zilizopiga hatua kiteknolojia.

“Tujipime na nchi ambazo zimeshatutangulia, tujiulize tutawafikiaje. Itakapofika wakati ambapo taarifa zote za mlipa kodi zinapatikana kwa urahisi na kwa wakati, ufanisi wa mamlaka ya mapato utaongezeka kwa kiasi kikubwa. Hivyo bado kuna haja ya kuendelea kuimarisha mifumo yetu,” amesema Waziri Khamis.

Uzinduzi wa mfumo wa IDRAS unaashiria hatua kubwa ya TRA katika mageuzi ya kidijitali ya ukusanyaji wa kodi nchini yakilenga kupunguza gharama za uendeshaji na kuimarisha mazingira rafiki kwa walipa kodi, hatua inayotarajiwa kuchochea ukuaji wa uchumi na kuongeza ufanisi wa taasisi hiyo kwa ujumla.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV