15 washikiliwa, msako wenye magari namba SSH 2530

September 4, 2025 6:27 pm ยท Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Muliro asisitiza kuwa kutumia namba hizo ni kosa kisheria

Dar es salaam. Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu 15 kwa tuhuma za kuendesha magari yenye namba SSH 2530, kinyume na sheria. Hatua hiyo ni mwendelezo wa operesheni ya kuhakikisha maagizo yaliyotolewa awali kuhusu marufuku ya namba hizo yanatekelezwa ipasavyo.

Akizungumza leo Alhamisi, Septemba 4, 2025, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amesema watuhumiwa tayari wamekamatwa huku msako dhidi ya wengine ukiendelea.

โ€œMtu yeyote anayebandika namba hizo, baada ya kufuatiliwa kwenye mifumo ya usajili wa namba, hili ni kosa kisheria,โ€ amesema Muliro.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amesema watuhumiwa tayari wamekamatwa huku msako dhidi ya wengine ukiendelea. Picha | Mwananchi.

Kwa mujibu wa Muliro, watu hao wamekamatwa kwa mujibu wa Kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Usalama Barabarani, Sura ya 168 Marejeo ya 1973 yaliyorekebishwa mwaka 2023, ambayo inaeleza kuwa ni kosa la jinai kwa mtu yeyote kuendesha chombo cha moto bila namba halali za usajili na yeyote anayekiuka hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

โ€œTunaendelea kusisitiza kuwa ni makosa na suala hili ni kinyume cha sheria kwa sababu namba hizo hazipo,โ€ amesisitiza Muliro.

Itakumbukwa kuwa Agosti mwaka huu, Jeshi la Polisi Tanzania kupitia Msemaji wake, David Misime, lilitangaza marufuku ya matumizi ya namba hizo na kuwataka wamiliki wa magari kuondoa ifikapo Septemba 1, 2025.ย 

Kutoka kwa marufuku ya Jeshi la Polisi kumekuja hiyo mara baada ya vyombo mbalimbali vya moto kuonekana vikitumia namba hiyo hivi karibuni jambo lililozua mijadala hususan katika majukwa mbalimbali ya mitandao ya kijamiii huku wengine wakihusisha utumiaji wa namba hizo na siasa katika kipindi kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW